Maendeleo ya kweli yatapatikana wanawake na wasichana wakiwa huru- Guterres
Ukatili dhidi ya wanawake na wasichana ni janga la kimataifa, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres wakati akihutubia tukio maalum la siku ya kimataifa ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake lililofanyika kwenye makao makuu ya umoja huo jijini New York, Marekani hii leo.