Wanawake walikuwa na mchango mkubwa katika kuandikwa kwa tamko la haki za binadamu
Wiki ijayo, dunia itaadhimisha miaka 70 ya tamko la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu. Ingawa historia ya dunia inaonekana kuwasahau wanawake, mtafiti wa masuala ya haki za binadamu Dkt Rebecca Adami katika kitabu chake cha ‘Wanawake na tamko la haki za binadamu’ anasema wanawake walikuwa na mchango mkubwa katika kuliandaa na kulitekeleza tamko hilo.