Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mlinda amani wa UNMISS akishika doria katika barabra karibu na Bentiu, jimbo la Unity, Sudan Kusini.
UNMISS Photo

Vikosi vya Umoja wa Mataifa Sudan Kusini vinawapeleka wanafunzi shuleni na kuwarudisha nyumbani wakati wa mitihani.

Walinda amani Sudan Kusini wasindikiza wanafunzi shuleni na kuwarudisha nyumbani wakati wa mitihani.Polisi waliopo kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini  wamepewa jukumu la kuwasindikiza wanafunzi hadi kwenye kituo cha mtihani kwenye mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba.  Usindikizaji huo unafanyika Kwa wiki mbili ambapo askari hao wataendelea kuwapeleka na kuwarudisha wanafunzi kufanya mitihani yao kwa usalama.

Sauti
1'57"
Walinda amani kutoka Chad wakipiga doria katika mitaa ya Kidal nchini Mali.(maktaba Desemba 2016)
MINUSMA/Sylvain Liecht

Walinda amani 10 kutoka Chad wauawa Kidal, Mali kufuatia shambulio

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali shambulizi dhidi ya kambi ya askari walinda amani wa Umoja wa Mataifa huko Aguelhok, eneo la Kidal nchini Mali leo Jumapili asubuhi, ambapo askari 10 kutoka Chad wameuawa na wengine 25 wamejeruhiwa. Katika shambulio hilo, vikosi vya MINUSMA vilijibu mashambulizi na baadhi ya waasi wameuawa.

Laurent Gbagbo na Charles Blé Goudé wakiwa mahakamani huko The Hague Uholanzi leo tarehe 15 Januari 2019 wakati hukumu ikisomwa. Wameachiwa huru.
ICC-CPI

ICC yawaachia huru Gbagbo na Blé Goudé

Mahakama ya kimataifa ya makossa ya jinai, ICC leo imemwachia huru rais wa zamani wa Côte d'Ivoire Laurent Gbagbo na aliyekuwa mkuu wa vijana Charles Blé Goudé baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha pasipo shaka mashtaka yote dhidi yao. Arnold Kayanda na taarifa zaidi.

Sauti
1'49"