Dau la plastiki, Flipflopi safarini kutoka Kenya hadi Zanzibar
Hatimaye dau la plastiki limeanza safari yake ya kilometa 500 kutoka Mombasa Kenya hadi Zanziabar Tanzania. Tumezungumza na mjenzi wake Ali Skanda
Hatimaye dau la plastiki limeanza safari yake ya kilometa 500 kutoka Mombasa Kenya hadi Zanziabar Tanzania. Tumezungumza na mjenzi wake Ali Skanda
Baraza la wakimbizi duniani, WRC limetoa wito kufanyike mabadiliko katika mifumo suala la wakimbizi duniani kwa ajili ya kulinda maslahi ya watu waliolazimika kukimbia ikiwemo walio wakimbizi wa ndani na jamii zinazowahifadhi.
Jukwaa la uchumi duniani likiendelea huko Davos nchini Uswisi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameweka bayana changamoto zinazokabili dunia hivi sasa akisema jawabu muhimu ni ushirikiano wa kimataifa ambao chombo anachoongoza ndio msingi wake. Assumpta Massoi na taarifa zaidi.
Leo Januari 24 ni siku ya kimatifa ya elimu duniani ambayo inaadhimishwa kwa mara ya kwanza tangu kupitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwezi Desemba mwaka jana kwa kutambua umuhimu wa elimu katika kubadili dunia na kufikia ajenda ya 2030 ya maendeleo endelevu.
Walinda amani Sudan Kusini wasindikiza wanafunzi shuleni na kuwarudisha nyumbani wakati wa mitihani.Polisi waliopo kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini wamepewa jukumu la kuwasindikiza wanafunzi hadi kwenye kituo cha mtihani kwenye mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba. Usindikizaji huo unafanyika Kwa wiki mbili ambapo askari hao wataendelea kuwapeleka na kuwarudisha wanafunzi kufanya mitihani yao kwa usalama.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali shambulizi dhidi ya kambi ya askari walinda amani wa Umoja wa Mataifa huko Aguelhok, eneo la Kidal nchini Mali leo Jumapili asubuhi, ambapo askari 10 kutoka Chad wameuawa na wengine 25 wamejeruhiwa. Katika shambulio hilo, vikosi vya MINUSMA vilijibu mashambulizi na baadhi ya waasi wameuawa.
Masuala ya hofu kuwa mtaji wa kisiasa, kauli za chuki, ukosefu wa usawa, ushirikiano wa kimataifa, mabadiliko ya tabianchi, maandamano huko Sudan na kwingineko duniani ni miongoni mwa mambo ambayo yamebeba mkutano kati ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na waandishi wa habari hii leo mjini New York, Marekani.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametaja maeneo matatu ya utekelezaji kwa mwaka huu wa 2019.
Mahakama ya kimataifa ya makossa ya jinai, ICC leo imemwachia huru rais wa zamani wa Côte d'Ivoire Laurent Gbagbo na aliyekuwa mkuu wa vijana Charles Blé Goudé baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha pasipo shaka mashtaka yote dhidi yao. Arnold Kayanda na taarifa zaidi.
Dau la kijadi lililotengenezwa na taka za plastiki zilizookotwa pwani ya Kenya na miji mbalimbali litaanza safari yake ya kwanza tarehe 24 mwezi huu kutoka mji mkongwe wa Lamu nchini Kenya hadi mji mkongwe huko Zanzibar nchini Tanzania tarehe 7 mwezi ujao, ikiwa ni safari ya umbali wa kilometa 500.