Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Chakula kinachohitajika sana kikisambazwa na WFP huko Cité Soleil, Haiti.
© WFP/Tanya Birkbeck

Licha ya hali tete ya usalama, WFP yafanikiwa kufikisha Msaada wa chakula nchini Haiti

Licha ya machafuko na mashambulizi yanayofanywa na makundi yenye silaha huko nchini Haiti, shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani limeendelea kuimarisha operesheni zake katika mji mkuu wa Port-au-Prince na kusaidia jamii zilizoathiriwa na ghasia ambapo kwa mwezi Mei shirika hilo limeweza kuwafikia zaidi ya watu 93,000.

Sauti
3'23"
Watu milioni moja wamelazimika kukimbia katika muda wa wiki tatu zilizopita huku mashambulizi makubwa ya mabomu yakiendelea huko Rafah kusini mwa Gaza.
© UNRWA

Vita Gaza imemong’onyoa utangamano wa kijamii - OCHA

Kadri siku zinavyozidi kusonga na mashambulizi yakiendelea huko Gaza, nafasi iliyosalia kwa ajili ya raia wa Gaza inazidi kuwa finyu huku mazingira ya maisha yakimong’onyoa utangamano wa kijamii amesema Afisa mwandamizi wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura, OCHA kwenye eneo hilo la wapalestina linalokaliwa na Israeli.

Wahamiaji wa Afrika Mashariki waliojaribu kuvuka bahari ya Mediterania wanaokolewa na jeshi la wanamaji la Italia huko Sicily.
© UNICEF/Gideon Mendel

Kuna mapungufu makubwa katika huduma za ulinzi kwenye njia za uhamiaji kutoka Afrika hadi Ulaya: UNHCR

Ukosefu wa huduma za ulinzi katika njia kuu zinazotumiwa na wakimbizi na wahamiaji wakitokea Afrika kuelekea Ulaya ni jambo la kutisha na  limekuwa baya zaidi katika miaka ya hivi karibuni, kulingana na ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa mataifa  la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR ambayo inaangazia mahitaji makubwa na hatari wanazokabiliana nazo.

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu kwenye ujumbe wa Umoja huo wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO wakiwa kwenye doria katika kijiji cha Logo mji wa Djugu jimboni Ituri .
MONUSCO

Walinda amani wa UN waweka doria kali mashariki mwa DRC baada ya kuibuka mapigano

Katika kukabiliana na hali ya mapigano makali yaliyoibuka tena mwishoni mwa wiki kati ya kundi lenye kujihami kwa silaha M23 na Jeshi la DR Congo (FARDC), walinda amani wa Umoja wa Mataifa kwa uratibu wa FARDC, wameweka doria karibu na Kanyabayonga kusaidia baadhi ya wanaume, wanawake na watoto 150,000 waliokimbia makazi yao katika siku za hivi karibuni mashariki mwa nchi.