GAZA: Janga laongezeka, misafara yenye misaada ‘yagonga mwamba’
Wakati kukiwa na ripoti ya kwamba Israel inaendelea na mashambulizi ya kutokea angani huko kusini na kati mwa Gaza huku mashambulizi ya maroketi yakimiminika ndani ya Israel kutoka Gaza, mashirika ya Umoja wa Mataifa ya kusambaza misaada ya kibinadamu yamesema kwa siku tatu mfululizo hayajaweza kusambaza misaada muhimu eneo la kati na kaskazini mwa eneo hilo lililozingirwa.