Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Shehena ya mablanketi 4,000 ikiwa inawasilishwa kwenye hospitali mbili zilizoko kusini mwa Gaza mwezi Desemba mwaka 2023 (Maktaba)
© UNICEF/Eyad El Baba

GAZA: Janga laongezeka, misafara yenye misaada ‘yagonga mwamba’

Wakati kukiwa na ripoti ya kwamba Israel inaendelea na mashambulizi ya kutokea angani huko kusini na kati mwa Gaza huku mashambulizi ya maroketi yakimiminika ndani ya Israel kutoka Gaza, mashirika ya Umoja wa Mataifa ya kusambaza misaada ya kibinadamu yamesema kwa siku tatu mfululizo hayajaweza kusambaza misaada muhimu eneo la kati na kaskazini mwa eneo hilo lililozingirwa. 

Mashambulizi dhidi ya meli za kibiashara katika Bahari ya Shamu yametatiza sana usafirishaji kwa njia ya maji kimataifa. (maktaba)
© Unsplash/Angus Gray

Umoja wa Mataifa waonya kuhusu athari za kuongezeka shughuli za kijeshi katika Bahari ya Shamu

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linafanya mkutano wake wa kwanza wa wazi kuhusu mashambulizi yanayoendelea kufanywa na waasi wa Houthi katika Bahari ya Shamu, ambayo yanazidi kuwa tishio kwa biashara ya kimataifa na uthabiti wa eneo zima huku vita kati ya Israel na wapiganaji wa Palestina huko Gaza vikiendelea. Fuatilia mkutano kwenye UN Web TV.

Mtaalamu Maalum wa Umoja wa Mataifa anayeshughulika na masuala ya mateso, na Adhabu nyingine za Kikatili, za Kinyume cha utu au za Kushusha hadhi, Alice Jill Edwards.
UN Video

Wataalamu wa UN wapinga utekelezaji wa hukumu ya kifo kwa kutumia gesi ya nitrojeni hypoxia

Wataalamu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa akiwemo Alice Jill Edwards, anayeshughulikia masuala yanayohusu mateso, na Adhabu nyingine za Kikatili, za Kinyama au ya Kushusha, hadhi leo Januari 3 mjini Geneva-Uswisi wameelezea wasiwasi wao kuhusu kukaribia kutekelezwa kwa hukumu ya kifo kwa kutumia gesi ya nitrojeni hypoxia dhidi ya Kenneth Eugene Smith hapa nchini Marekani.  

Sauti
2'1"
Mtoto mwenye umri wa miaka minane akisubiri mgao wa chakula huko Rafah, kusini mwa Gaza
© UNICEF/Abed Zagout

GAZA: Mashambulizi yakishamiri, njaa na magonjwa navyo vyatawala

Mashirika ya Umoja wa Mataifa ya usaidizi wa kiutu hii leo Jumanne yameendelea kuelezea wasiwasi wao mkubwa juu ya hatma ya raia walionasa kwenye mapigano huko Ukanda wa Gaza wakati huu kukiwa na ripoti ya kwamba jeshi la Israel limeendelea na mashambulizi kwenye miji ya kusin mwa Gaza ya Deir al Balah, Khan Younis na Rafah huku vikundi vya kipalestina vilivyojihami vikirusha makombora usiku kucha kuelekea Israel.