Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wahudumu wa afya ni kiungo muhimu katika kutokomeza saratani ya shingo ya kizazi
Pan American Health Organization

Udadavuzi: Saratani ya shingo ya kizazi 

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO limetangaza kuwa mwezi wa Januari ni mwezi wa kuhamasisha jamii kuhusu saratani ya shingo ya kizazi. Makala hii inaangazia kuhusu ugonjwa huo, unasababishwa na nini, tiba yake pamoja na jinsi ya kujikinga. 

Julienne Lusenge, mwanaharakati wa haki za binadamu wa Kongo ambaye ni rais wa kundi la Sofepadi na mkurugenzi wa Mfuko wa Wanawake wa Kongo wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu unyanyasaji dhidi ya wanawake katika migogoro. (Maktaba - 25 Febr…
UN Photo/ Jean Marc Ferré

Mahojiano: SOFEPADI ilivyomsaidia manusura wa ukatili wa kingono Ituri, nchini DRC

Ukatili wa kingono vitani ni jambo linalokumba wanawake, na wasichana Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Wanapobakwa na kupewa  ujauzito wengi wao hukosa pa kukimbilia kusaka msaada wa kiafya na kisaikolojia. Julienne Lusenge, mshindi wa tuzo ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu kwa mwaka 2023 kwa kutambua hilo mwaka 2000 aliunda SOFEPADI, shirika la kiraia la kusaidia wanawake na watoto waliokumbwa na ukatili wa kingono na ubakaji. 

Shehena ya mablanketi 4,000 ikiwa inawasilishwa kwenye hospitali mbili zilizoko kusini mwa Gaza mwezi Desemba mwaka 2023 (Maktaba)
© UNICEF/Eyad El Baba

GAZA: Janga laongezeka, misafara yenye misaada ‘yagonga mwamba’

Wakati kukiwa na ripoti ya kwamba Israel inaendelea na mashambulizi ya kutokea angani huko kusini na kati mwa Gaza huku mashambulizi ya maroketi yakimiminika ndani ya Israel kutoka Gaza, mashirika ya Umoja wa Mataifa ya kusambaza misaada ya kibinadamu yamesema kwa siku tatu mfululizo hayajaweza kusambaza misaada muhimu eneo la kati na kaskazini mwa eneo hilo lililozingirwa. 

Mashambulizi dhidi ya meli za kibiashara katika Bahari ya Shamu yametatiza sana usafirishaji kwa njia ya maji kimataifa. (maktaba)
© Unsplash/Angus Gray

Umoja wa Mataifa waonya kuhusu athari za kuongezeka shughuli za kijeshi katika Bahari ya Shamu

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linafanya mkutano wake wa kwanza wa wazi kuhusu mashambulizi yanayoendelea kufanywa na waasi wa Houthi katika Bahari ya Shamu, ambayo yanazidi kuwa tishio kwa biashara ya kimataifa na uthabiti wa eneo zima huku vita kati ya Israel na wapiganaji wa Palestina huko Gaza vikiendelea. Fuatilia mkutano kwenye UN Web TV.

Mtaalamu Maalum wa Umoja wa Mataifa anayeshughulika na masuala ya mateso, na Adhabu nyingine za Kikatili, za Kinyume cha utu au za Kushusha hadhi, Alice Jill Edwards.
UN Video

Wataalamu wa UN wapinga utekelezaji wa hukumu ya kifo kwa kutumia gesi ya nitrojeni hypoxia

Wataalamu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa akiwemo Alice Jill Edwards, anayeshughulikia masuala yanayohusu mateso, na Adhabu nyingine za Kikatili, za Kinyama au ya Kushusha, hadhi leo Januari 3 mjini Geneva-Uswisi wameelezea wasiwasi wao kuhusu kukaribia kutekelezwa kwa hukumu ya kifo kwa kutumia gesi ya nitrojeni hypoxia dhidi ya Kenneth Eugene Smith hapa nchini Marekani.  

Audio Duration
2'1"