Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Jamie McGoldrick mratibu mkazi wa muda na misaada ya kibinadamu katika eneo linalokaliwa la Palestina  akikutana na watu waliotawanywa kwenye eneo la Rafah Kusini mwa Gaza
OCHA /oPt

Msaada unaoingia Gaza hautoshelezi matakwa ya watu milioni 2.2: Jamie McGoldrick

Katika mahojiano maalum na UN News kupitia njia ya simu yaliyofanyika kutoka Jerusalem leo Januari 13 Jamie McGoldrick, Naibu Mratibu Maalum wa Muda na Mratibu Mkazi, wa Ofisi ya Mratibu Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya mchakato wa amani ya Mashariki ya Kati UNSCO, amesema, "kuna hali ya mshtuko na kiwango cha kukata tamaa. Na nadhani kuna hali ya kutokuwa na tumaini huko pia, kwa sababuwatu wa Gaza hawaoni hatua yoyote kwa kile wanachokikabili mbele yao.”

Olga (kushoto) akiwa na mbwa na mtoto wake, waathirika wa vita inayoendelea nchini Ukraine.
UNHCR Video

Bila UNHCR sijui ningekaa wapi: Olga muathirika wa vita Ukraine

Kutana na Olga mwathirika wa vita inayoendelea nchini Ukraine ambaye baada ya nyumba yake kushambuliwa na kombora mjini Borodyanka alikataa tamaa ya Maisha lakini sasa mradi wa UNHCR wa kukarabati nyumba zilizoharibiwa na vita Ukraine umemfufulia matumaini ya Maisha yeye na mwanaye “Katika maisha mambo hayawezi kuwa mteremko tu, kuna wakati unapitia magumu na ukiwa na uvumilivu utayashinda.

Sauti
3'9"
Mikutano ya hadhara katika kesi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki
ICJ-CIJ/ Frank van Beek

Vita dhidi ya Hamas huko Gaza ni kitendo cha kujilinda, Israel yaiambia mahakama ya ICJ

Israel imekanusha vikali shutuma kuwa ina nia ya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina na kusisitiza kuwa ipo katika vita ambayo wao hawakuianzisha na wala hawakuitaka kufuatia hapo jana nchi ya Afrika kusini kuwasilisha kesi mbele ya mahakama ya Umoja wa Mataifa ya kimataifa ya haki ICJ wakitaka kukomesha mauaji ya raia huko Gaza. 

Sauti
3'4"
Banamwana Yvette Mfanyakazi wa Ofisi za Jiji na Kigali.
UNICEF

Tunapaswa kuhakikisha kunyonyesha maziwa ya mama kwa mtoto mahali pa kazi inawezekana – UNICEF Rwanda

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF Rwanda kwa kushirikiana na wadau kama Shirika la Taifa la Maendeleo ya Mtoto nchini humo, NCDA, wanatoa wito kwa sekta binafsi, taasisi za serikali, washirika, asasi za kiraia kuweka mazingira rafiki ya unyonyeshaji mahali pa kazi. Evarist Mapesa anaangazia faida ya moja ya vyumba vya kunyonyeshea mahali pa kazi jijini Kigali Rwanda. 

Sauti
2'34"