Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Aristote Muhawe ni mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akiishi katika makazi ya wakimbizi ya Kyangwali magharibi mwa Uganda. Hapa anasoma shule ya sekondari pamoja na wakimbizi kutoka Sudan Kusini.
UN News

Elimu na Amani: Wakimbizi waelezea jinsi elimu ilivyobadili mtazamo wao hasi dhidi ya watu wengine

Nafasi ya elimu katika kuchagiza amani miongoni mwa wakimbizi na  jamii zinazowahifadhi imedhihirika huko Uganda wilayani Kikuube magharibi mwa nchi ambako kuna makazi ya wakimbizi ya Kyangwali. Hilo limethibitika wakati huu dunia kesho Januari 24 ikiadhimisha siku ya elimu duniani maudhui yakiwa kujifunza kwa ajili ya amani. 

Kipepeo aina ya monarch hukusanya nekta kutoka kwenye mmea wa mbigili (thistle plant).
Unsplash/Sean Stratton

Bioanuwai: Ni nini, na tunawezaje kuilinda?

Umoja wa Mataifa na wadau wake ulimwenguni wanakabiliana na upotevu mkubwa wa wanyama na mimea, tarehe 23 Januari wanakutana jijini Nairobi, kenya kujadili jinsi ya kuepuka upotevu huo, katika mkutano mkuu ambao utaangazia bioanuwai ni nini, na jinsi gani Umoja wa Mataifa, unaweza kusaidia juhudi za kuwezesha asili kuishi na kustawi.

Mtoto mwenye umri wa miaka 3 anaendelea kupona baada ya kukatwa mguu wake kufuatia shambulizi la moja kwa moja la kombora nyumbani kwake katika mji wa Nuseirat katikati mwa Ukanda wa Gaza.
© UNICEF/Abed Zaqout

Mapigano Gaza sasa yanasambaa hospitali, hakuna njia ya kuingia wala kutoka: UN

Wakati mapigano makali  yakiendelea huko Gaza leo asubuhi ikiwa ni pamoja na mashambulizi yaliyoripotiwa dhidi ya hospitali katika mji wa kusini wa Khan Younis, wahudumu wa misaada wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa walionyesha wasiwasi mkubwa kwa wagonjwa na watu wengine wanaosaka matibabu ambao wamejikuta katikati ya mapigano hayo bila njia ya kuingia wala kutoka.

Mtoto aliyejeruhiwa anatunzwa katika Hospitali ya Nasser iliyoko Khan Younis.
© UNICEF/Abed Zaqout

Habari kwa ufupi: Gaza; Ukraine; Rohingya

Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA limeonya kwamba watu 570,000 wanakabiliwa na janga kubwa la njaa kutokana na kuendelea kwa mapigano makali huko Gaza, wahudumu wa misaada kunyimwa fursa ya kuwafikia wenye uhitaji na kukatwa kwa mawasiliano, sababu ambazo pia zimeathiri uwezo wa shirika hilo  kufikisha na kusambaza msaada kwa usalama kwa maelfu ya watu. Hivyo limetoa wito wa kuongezwa haraka fursa za usambazaji na ufikishaji wa misaada ya kibinadamu. 

Majanga yatokanayo mafuriko yanababisha usumbufu, majeruhi wengi na hasara kubwa za kiuchumi katika sehemu mbalimbali za dunia.
Dinga Bienvenue/Congo National Hydrological Service

Tahadhari za mapema kuhusu maji na majanga ni muhimu:WMO

Kikosi cha wataalamu kuhusu huduma za tahadhari ya mapema kimekutana katika Shirika la Umoja wa Mataifa la utabiri wa hali ya Hewa Duniani, WMO huko jijini Geneva, Uswisi, kutathimini hali ya  Jamhuri ya Congo Brazzaville, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na nchini Mauritius, ili kuendeleza mpango wa kimataifa wa kutoa tahadhari za mapema kwa wote na pia kuchukua hatua kuboresha usimamizi wa rasilimali za maji na kupunguza hatari zinazohusiana na maji.