Matendo ya Taliban kuwaweka kizuizini wanawake kwa sababu ya mavazi yakome: Wataalamu wa UN
Wataalamu wa Umoja wa Mataifa leo wameelezea wasi wasi wao kutokana na ripoti nyingi kwamba wanawake na wasichana wengi nchini Afghanistan wamewekwa kuzuizini kiholela na kufanyiwa vitendo viovu tangu mapema Januari mwaka huu 2024 kwa madai ya kukiuka kanuni za mavazi za Taliban kwa wanawake.