Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Maonesho ya bidhaa za kupambana na saratani kwenye kongamano la kwanza la taifa la saratani nchini Kenya.
UN News Nairobi/Thelma Mwadzaya

Licha ya kuweko kwa mbinu za kudhibiti, bado saratani yaendelea kuwa mzigo wa afya duniani

Takwimu mpya za Umoja wa Mataifa zinaonesha kuwa ugonjwa wa saratani umeendelea kuwa mzigo kubwa wa afya duniani na kusababisha vifo licha ya kuweko kwa mbinu za ugunduzi na matibabu, huku saratani  ya mapafu ikishika nafasi ya kwanza na ile ya titi ikishika nafasi ya pili na wadau wakitaka utashi wa kisiasa ili kutokomeza ugonjwa huo.

Timu za UNRWA zinaendelea kusambaza misaada ya kibinadamu huko Gaza.
© UNRWA

Habari kwa ufupi: Msaada wa kibinadamu Gaza; Wandishi wa Habari; Saratani

Kufuatia uamuzi wa nchi 16 wafadhili kusitisha utoaji fedha kwa shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia wakimbizi wa kipalestina UNRWA baada ya Israel kulishutumu shirika hilo kuwa wafanyakazi wake 12 walihusika katika shambulio lililotokea tarehe 7 Oktoba mwaka jana, Mkuu wa UNRWA Philipe Lazzarini amesema kuwa iwapo fedha zitaendelea kuzuiliwa, watalazimika kufunga operesheni zao ifikapo mwishoni mwa mwezi huu wa Februari. 

Familia ya watu waliohamishwa makazi yao huko Tabarre, Haiti wakusanyika kwenye tovuti.
© UNICEF/Ndiaga Seck

UNICEF: Watoto 170,000 nchini Haiti wafurushwa makwao

Wakati mzozo wa makundi yanayotumia silaha uliendelea kuongezeka nchini Haiti, shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF hii leo limeeleza idadi ya watoto waliokimbia makazi yao imefikia 170,000 na kutaja kuwa hiyo ni idadi kubwa ya kutisha inayoashirikia kuzidi kuzorota kwa usalama nchini humo huku watoto na familia zao wakizidi kuwa hatarini. 

Ujenzi wa madarasa nchini Mozambique yanayohimili hali mbaya za hewa ikiwemo vimbunga vinavyong’oa mapaa.
UN Habitat Mozambique

Iwe mvua iwe upepo mkali madarasa yetu ni salama: Mwanafunzi Msumbiji

Kila mwaka, Msumbiji hukabiliwa na matukio ya hali mbaya za hewa kupindukia kama vile vimbunga na mafuriko, matukio ambayo husababisha uharibifu wa shule na hatimaye watoto kushindwa kujifunza. Hata hivyo, ujenzi wa madarasa yanayohimili matukio kama vile pepo kali na mafuriko umeleta nuru na matumiani kwa watoto, wazazi na walimu. Madarasa haya yanawezesha watoto kubakia salama hata wakati wa mvua na upepo mkali. Hali hii ni uwekezaji wa kudumu kwani ni  hakikisho kwa watoto kuendelea kupata elimu na mustakabali wao kuwa bora. 

Sauti
4'11"
Timu za UNRWA zinafanya kazi usiku kucha kusambaza chakula kwa Wapalestina waliokata tamaa.
© UNRWA

'Hatuwezi kuwatelekeza watu wa Gaza': wakuu wa mashirika ya UN na mashirika yasiyo ya kiserikali

Wakati mapigano makali na mashambulizi ya makombora yaliendelea huko Khan Younis kusini mwa Gaza usiku wa kuamkia leo Jumatano, wasaidizi wakuu wa Umoja wa Mataifa na wakuu wa mashirika yasiyo ya kiserikali wameonya juu ya ‘matokeo mabaya’ ya kutofadhili shughuli za Shirika la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina UNRWA ambalo linashutumiwa kushirikiana na wanamgambo wa kipalestina wa Hamas.