Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mtoto mdogo akipokea matibabu katika kituo cha matibabu ya kipindupindu huko Kivu Kaskazini, DR Congo.
© UNICEF/Jospin Benekire

UNICEF yaisaidia DRC katika mafuriko mabaya kuhushudiwa kwa miaka 60

Mjini Kinshasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na wadau wengine wa misaada ya kibinadamu wamesema wanafanya kila liwezekanalo kuwasaidia waathirika wa mafuriko mabaya zaidi nchini humo yaliyosababisha kina cha mto Congo kufurika katika kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa katika kipindi cha zaidi ya miaka 60.