Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Rais William Samoei Ruto wa Jamhuri ya Kenya akihutubia mjadala mkuu wa kikao cha 78 cha Baraza Kuu.
UN Photo/Cia Pak

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa lifanyiwe marekebisho - Rais Ruto

Takwa la muda mrefu la viongozi wengi hususani kutoka Barani Afrika la Baraza la Usalama la Umoja wa lililoundwa tarehe 25 Octoba mwaka 1945 kufanyiwa marekebisho makubwa limeendelea kuchukua nafasi katika hotuba za viongozi wa ngazi za juu wanaohutubia katika mkutano wa 78 wa Baraza Kuu wa Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani ambapo hii leo Rais wa Kenya amesema sababu zote za kulifanyia marekebisho zipo wazi. 

Madina Jubilate Kimaro, Balozi wa Mazingira wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniani, UNICEF nchini Tanzania.
UN/Assumpta Massoi

Samadi ya ng’ombe yachukua nafasi ya mkaa wa miti - Madina

Je umewahi kuona changamoto ukaigeuza fursa si kwako tu bali kwa wengine pia? Hiyo imemtokea Madina Jubilate Kimaro, msichana mwenye umri wa miaka 19 nchini Tanzania ambaye akiwa kwa bibi au nyanya yake jijini Dar es salaam nchini humo aliwaza na kuwazua kuona ni kwa vipi anaweza kutumia samadi ya ng’ombe kuwa bidhaa ya kusaidia kukabili mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
6'24"
Rais wa Zimbabwe Emmerson Dambudzo Mnangagwa wakati akihutubia mkutano wa 78 Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani
UN Photo/Cia Pak

Acheni kutumia vikwazo vya kimataifa kama silaha - Rais Mnangangwa

“Tunalaani vikwazo vinavyowekwa na nchi tajiri kwa nchi kama zimbabwe na Cuba ambavyo ni haramu na vinatumiwa kama nyenzo ya sera za kigeni ya mataifa tajiri kwani vikwanzo hivyo vinatatiza uaminifu, mshikamano na umoja wa kimataifa.“ Amesema leo Rais wa Zimbabwe Emmerson Dambudzo Mnangagwa wakati akihutubia mkutano wa 78 Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani.

Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wakifanya doria ya usiku huko Bentiu, Sudan Kusini.
UNMISS/Gregório Cunha

Habari kwa ufupi na yanayoendelea UNGA78

Leo ni siku ya tatu ya mjadala mkuu wa mabaraza kuu la Umoja wa Mataifa UNGA78 ambapo wakuu wa nchi na serikali wanaeendelea kutoa hotuba zao kutathimini changamoto na hatua zilizopigwa katika utekelezaji wa ajenda za Umoja wa Mataifa, na miongoni watakaopanda katika mimbari leo kutoka Afrika ni Rais wa Kenya, Burundi, Sudan Kusini, Zimbabwe, Malawi, Sudan na makamu wa Rais wa Uganda na Tanzania.