Viongozi wa dunia na ahadi mpya ya kutokomeza TB
Vifijo na nderemo vilisikika kwenye moja ya kumbi za mikutano kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani hii leo baada ya wawakilishi wa serikali, wataalamu wa afya na wawakilish iwa mashirika ya kiraia kupitisha azimio la kisiasa lenye lengo la kutokomeza Kifua Kikuu au TB ifikapo mwaka 2030 ambapo pamoja na mambo mengine linalenga kufikia asilimia 90 ya watu na huduma za kinga na tiba dhidi ya TB.