Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mtoto kutoka Mtedera Zambia akipweza chanjo ya kipindupindu
Picha ya Gavi Alliance/Duncan Graham-Rowe

Mashirika ya UN yahaha kuisaidia Zambia dhidi ya kipundupindu 

Baada ya mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu nchini Zambia, Kikosi Kazi cha Umoja wa Mataifa kikiongozwa na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini humo Beatrice Mutali wanaisaidia serikali ya Zambia kukabiliana na ugonjwa huo ambao umetokea huku kukiwa na mafuriko makali yaliyowafurusha zaidi ya watu 170,000 katika wilaya 22 za nchi hiyo barani Afrika.  

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu wakimbizi Filippo Grandi akiwa ziarani Ziara ya wakimbizi wa Eritrea waliokimbia makazi yao kutokana na vita katika jimbo la Tigray nchini Ethiopia
© UNHCR/Samuel Otieno

Nuru ya amani iking’ara Ethiopia, UNHCR yataka majawabu ya kudumu ya usaidizi kwa wakimbizi

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu wakimbizi Filippo Grandi, amehitimisha ziara yake ya siku tatu nchini Ethiopia na kusisitiza msimamo wake wa kuunga mkono hatua za kiutu kwa wakimbizi na wakimbizi wa ndani nchini Ethiopia, na kufanya kazi ili kupata majawabu ya muda mrefu ikiwemo wale waliofurushwa makwao kutokana na ukame na madhara ya mabadiliko ya tabianchi. 

Chakula kinasambazwa kwa watu waliokimbia makazi yao baada ya tetemeko la ardhi huko Aleppo, Syria.
© Al-Ihsan Charity

Tunataka kuwafikia waathirika wote japo kuna kikwazo cha usalama katika baadhi ya maeneo - WFP Syria

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanaendelea kupeleka na kusambaza misaada nchini Uturuki na Syria ili kusaidia walioathiriwa na matetemeko makubwa ya ardhi yaliyotokea Jumatatu wiki hii na kujeruhi, kuua maelfu na kuharibu miundombinu. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) lina lengo la kuwafikia watu nusu milioni katika nchi zote mbili ijapokuwa kuna changamoto za kiusalama katika baadhi ya maeneo.

Sauti
2'59"