Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Begi la sola lililotengenezwa kwa kutumia taka mali. Kipande cha sola kimeunganishwa na waya inayopokea nishati ya jua na kuingiza katika taa maalumu ambayo usiku hutumika kwa ajili ya kujisomea
UN News

Soma Bag: Mabegi ya mgongoni yanayotumia sola mkombozi kwa wanafunzi

Lengo namba nne la Malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa SDGs linazungumzia juu ya elimu bora, yenye usawa na kutoa fursa kwa wote, na hicho ndicho kinachofanyika jijini Mwanza kaskazini Magharibi mwa Tanzania ambapo vijana wamebuni mradi wa mabegi yanayokusanya nishati ya jua ili kuwasaidia wanafunzi waishio vijijini kujisomea nyakati za usiku.

WFP na serikali ya Madagascar zaungana mikono kubadilisha jamii za vijijini kusini mwa Madagascar.
© WFP Madagascar

Mradi wa RRT wa paneli za sola waangaza nuru Kusini mwa Madagascar:WFP

Kupitia mradi wa mabadiliko ya haraka vijijini (RRT) shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP na wadau wake wameanzisha kituo maalum cha paneli za sola ambacho ni chanzo kikuu na endelevu cha maji na teknolojia ya mawasiliano ICT katika maeneo ya vijijini nchini Madagascar, hatua inayoruhusu upatikanaji wa huduma muhimu kama vile nishati, maji na mitandao ya kijamii kwa wakazi wa jamii hizo na kwa njia inayojali mazingira.

Sauti
2'35"