UNGA77 yafunga pazia, Afrika yasema sasa ni wakati wa kuwa na ujumbe wa kudumu
Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA77 umekunja jamvi kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa ukiwa na maudhui: Wakati muhimu: Majawabu ya kuleta marekebisho kwa changamoto zinazofungamana. Katika siku 6 za mjadala huo nchi za Afrika zilitumia fursa kuhoji marekebisho gani yanawezekana bila kurekebisha chombo hicho ambacho kura yenye maamuzi ya msingi inamilikiwa na wanachama 5 kati ya 193, ikiwa ni miaka 77 tangu kuudwa kwake.