Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UN Video

Vijana tunachagiza mabadiliko ya kisera ili kulinda bahari - Nancy Iraba

Mkutano wa pili wa kimataifa kuhusu bahari unaendelea huko Lisbon, Ureno. Mkutano huu umeanza tarehe 27 mwezi huu wa Juni na utamalizika tarehe 1 Julai 2022. Kabla ya kuanza kwa kikao cha ngazi ya juu, mkutano ulitanguliwa na jukwaa la vijana likileta pamoja wanaharakati na wachechemuzi vijana kuhusu masuala ya baharí wakionesha ubunifu wao wa jinsi ya kutatua dharura ya baharí, kama alivyooiita Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres .Miongoni mwa washiriki ni kijana Nancy Iraba mwanasayansi wa masuala ya bahari kutoka Chuo Kikuu cha Dare es salaam nchini Tanzania. Hapa akihoijwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa anaelezea jukwaa linajikita na nini.

Sauti
1'32"
Ufunguzi wa mkutano kuhusu bahari huko Lisbon, Ureno 27 Juni 2022
UN /Eskinder Debebe

Bahari inatupeleka popote, tuitunze- Guterres

Mkutano wa pili wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari umeanza leo huko Lisbon Ureno ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ni lazima kubadili mwelekeo na mwenendo wa shughuli za binadamu kwa bahari la sivyo uchafuzi wa bahari utavuruga harakati zote za kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs

Sauti
2'3"