Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UN/ Anold Kayanda

UN haiwezi kusahau Pembe ya Afrika

Ukame unaochochewa na mabadiliko ya tabianchi umesababisha watu takribani milioni 15 katika eneo la Pembe ya Afrika kukosa uhakika wa kupata chakula. Sasa Umoja wa Mataifa unafanya nini? Joyce Msuya, Msaidizi wa Katibu Mkuu na Naibu Mkuu wa OCHA anafafanua akianza kwa kueleza taswira ya njaa katika eneo hilo hususan Kenya, Ethiopia na Somalia.

Sauti
10'34"
Mapigano ya kikabila katika eneo la Jonglei nchini Sudan Kusini yamesababisha utekaji nyara na mauaji. (Maktaba))
UNMISS

Mzozo wa wakulima na wafugaji Sudan Kusini wasababisha vifo vya zaidi ya watu 130 

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini UNMISS umechukua jukumu la kuwaleta pamoja raia na vyombo vya usalama vya serikali ili kuzungumza na kusaka amani kufuatia migogoro baina ya wakulima wakazi wa Magwi na wafugaji wanaohamahama, mapigano ambayo yamesababisha vifo vya watu 130 pamoja na kuchochea vitendo vya udhalilishaji.

Sauti
2'38"
Utepe mwekundu- ishara ya kimataifa ya kampeni ya kupambana na VVU na UKIMWI
Public Health Alliance/Ukraine

Elimu ya afya ya uzazi haipaswi kuwa aibu – Tumaini Community Services Mbeya Tanzania 

Nchini Tanzania, Shirika la Tumaini Community Services linatekeleza mradi wa ‘Dreams’ yaani ‘Ndoto’ katika wilaya ya Mbeya mjini, Kyela na Mbarari mkoani Mbeya kwa ufadhili wa mfuko wa rais wa Marekani wa harakati za kupambamba na UKIMWI, PEPFAR kanda ya Tanzania, lengo likiwa kuwawezesha vijana balehe elimu ya afya ya uzazi, elimu ya kujitambua na elimu ya kiuchumi ili kupunguza maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI.

Sauti
2'50"