Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Brigedia Jenerali George M. Itang'are, Mwambata wa Kijeshi Ubalozi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa (katikati) akiwa ameshikilia moja ya nishani ya Dag Hammarskjöld ambayo walitunukiwa walinda amani wawili wa Tanzania w
Ofisi ya Mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa, New York, Marekani.

Mashujaa watanzania wawili miongoni mwa waliotunukiwa medali ya Dag Hammarskjold

Kuelekea siku ya kimataifa ya walinda amani ambayo itaadhimishwa Jumapili hii tarehe 29 Mei, Umoja wa Mataifa umetoa medali kuwatambua na kuwaenzi walinda amani majasiri. Miongoni mwa medali zilizotolewa ni ya Dag Hammarskjoldna kati ya waliotunukiwa ni askari wawili wa Tanzania waliouawa mwaka 2021 wakiwa katika majukumu ya ulinzi wa amani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.

Sauti
2'27"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akizungumza na waandishi wa habari pamoja na Rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine
UN /Eskinder Debebe

Guterres awaambia waukraine 'dunia inawaona' huku akiahidi msaada zaidi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameielezea Ukraine kama "kitovu cha maumivu na zahma isiyovumilika", alipozungumza na wanahabari leo mjini Kyiv akiwa pamoja na mwenyeji wake rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine na kuahidi kuongeza msaada kwa watu wa taifa hilo huku kukiwa na mateso makubwa , na mamilioni ya watu wamekimbia makazi yao kutokana na uvamizi wa Urusi. 

Nataliia Vladimirova na binti yake Oleksandra au Sasha kwenye umri wa miaka 4 wakiwa mjini Lisbon ,Ureno ambako waliwasili tarehe 14 Machi 2022 wakikimbia vita nchini mwao Ukraine
UN News/Leda Letra.

Ukraine: Hofu yangu ni mume wangu- Nataliia

Nataliia Vladimirova alikimbia nyumbani kwake Kharkiv, Ukraine, siku ya kwanza tu Urusi  ilipovamia nchi yao tarehe 24 mwezi Februari, 2022, akiambatana na binti yake Oleksandra mwenye umri wa miaka 4 pamoja na mama mkwe wake. Wao ni miongoni mwa maelfu ya wakimbizi wa Ukraine waliopata hifadhi ya muda nchini Ureno . Akihojiwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa huko Ureno, Nataliia al maaruf Natasha, anasimulia simulizi wa yale aliyopitia ikiwemo kugawanyika kwa familia sambamba na kupoteza wengine. 

 

Raia 11 wa Rwanda wakiwemo wapiganaji wa zamani 4 na wategemezi wao wakiwa wamepiga picha ya pamoja katika kituo cha mpito cha Munigi, Goma jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC kabla ya kuondoka kurejea nyumbani 24 February 2022.
UN/Eskinder Debebe

Tamu-chungu ya wapiganaji wa zamani kurejea nyumbani Rwanda baada ya mapigano msituni DRC

“Mke wangu niliyempata wakati napigana porini, alijifungua mtoto, sasa nikaona maisha ya kukimbia huku na kule porini na familia hayawezekani tena bora nirudi nyumbani Rwanda nikalee familia yangu.” Ni Mukeshimana Jean-Nepo, mpiganaji wa zamani wa kikundi cha Raiya Mutomboki nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akizungumza kwa furaha siku ya kurejea nyumbani Rwanda tarehe 24 mwezi Februari mwaka 2022.