Watoto wangu hawatemewi tena mate, nashukuru UN- Mama Kasereka
Watoto wangu hawatemewi tena mate, nashukuru UN- Mama Kasereka
“Nilianza kufanya shughuli za kujiuza mwili nikiwa na umri mdogo”, kwa masikitiko makubwa anaanza kueleza ambaye alipoteza wazazi akiwa mdogo na kukulia katika mazingira ya vita nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.
“Nilianza kufanya shughuli za kujiuza mwili nikiwa na umri mdogo”, kwa masikitiko makubwa anaanza kueleza ambaye alipoteza wazazi akiwa mdogo na kukulia katika mazingira ya vita nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC.
Ili kukisikiliza kisa cha mama huyu manusura wa unyanyasaji wa kingono katika maeneo yenye mizozo, ambaye pia ni mnufaika wa mfuko wa @UN unaoratibiwa na @UN_OSCSEA kupitia @MONUSCO nchini DRC, Bofya hapa https://t.co/OK9f1X19cB pic.twitter.com/ykki1z8rEE
HabarizaUN
Masika Kasereka anasema tangu wakati huo hadi wakati ambapo alianza kunufaika na mfuko wa ufadhili wa Umoja wa Mataifa wa kuwasaidia waathirika wa ukatili wa kijinsia na kingono, SEA ulioanzishwa na Umoja wa Mataifa mwaka 2016, maisha yake yalikuwa ya kutangatanga na hata ana watoto wawili ambao kwa miaka yote hiyo hawakuwahi kukanyaga shuleni.
Umoja wa Mataifa umekuwa ukiendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali kupitia ufadhili wa mfuko wake huo na mmoja wa wanufaika ni huyu Masika kutoka Bukavu ambao ni mji mkuu wa jimbo la Kivu Kusini. Yeye ameaanza kuona mwanga katika maisha yake ambayo awali yalikuwa yamegubikwa na kiza kizito, alikuwa kahaba tangu mdogo, yeye akitumia neno kimbaraga kuelezea hiyo shughuli ya kujiuza mwili.
Hatua mpya katika maisha yake ilikuja pale ambapo alikutana na kusaidiwa na shirika la Kavumu chini ya Mama Zawadi Bagaya ambaye anapata ufadhili kupitia mfuko huo wa Umoja wa Mataifa. Amewasaidia wanawake kupata ujuzi mbalimbali ikiwemo ushonaji wa nguo, au Kutur, wakitengeneza nguo za vitenge akitumia neno Tantileri na pia batiki.