Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UN Photo/Violaine Martin (file)

Ni wakati wa kupiga kengele ya dharura- Guterres

“Ni wakati wa kupiga kengele ya dharura”, amesema Katibu Mkuu wa UN katika mahojiano maalum na Idhaa ya Umoja wa Mataifa siku chache kabla ya kuanza kwa Mjadala wa Juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Akihojiwa na Assumpta Massoi wa UN News, António Guterres amegusia ushirikiano wa kimataifa, harakati za utoaji wa chanjo dhidi ya COVID-19 duniani, mabadiliko ya tabianchi, usawa wa jinsia, viijana, amani na usalama barani Afrika na duniani kwa ujumla.

Sauti
9'34"
UN inasema mgao wa chanjo dhidi ya COVID-19 kwa nchi zinazoendelea kama Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC unapaswa kuimarishwa.
© UNICEF/Zoe Mangwinda

Bila chanjo za kutosha, Afrika itageuka mazalia ya aina mpya za virusi vya COVID-19- WHO

Wakati mfumo wa Umoja wa Mataifa COVAX wa kusaka na kusambaza chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona au COVID-19, ukilazimika kukata mgao wa chanjo takribani milioni 150 kwa bara la Afrika kwa mwaka huu wa 2021, inaelezwa kuwa bara hilo linakabiliwa na uhaba wa dozi milioni 500 ambazo zingaliliwezesha kufikia lengo la kupatia chanjo asilimia 40 ya wakazi wake.

 

Watu wakiwa katika mto uliofurika Magharibi mwa Haiti baada ya daraja kusombwa na maji kufuatia kimbunga Matthew
MINUSTAH/Logan Abassi

Muda unatutupa mkono kuepuka janga la mabadiliko ya tabianchi:UN Ripoti 

Kupunguzwa kwa muda kwa uzalishaji wa hewa ukaa kulikosababishwa na masharti ya kimataifa ya watu kusalia majumbani wakati wa janga la corona au COVID-19 hakukupunguza kasi ya kuendelea kwa mabadiliko ya tabianchi. Viwango vya gesi chafuzi vimevunja rekodi, na dunia iko njiani  kuelekea hatari joto kali la kupindukia,  imeonya ripoti ya mabadiliko ya tabia nchi iliyotolewa leo na mashirika  mbalimbali.