Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ni wakati wa kupiga kengele ya dharura- Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres.

Huwezi kupewa madaraka bali unayatwaa, kwa hiyo tunahitaji wanawake kupigania haki zao kikamilifu

António Guterres , Katibu Mkuu wa UN

UN Photo/Violaine Martin (file)
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres.

Ni wakati wa kupiga kengele ya dharura- Guterres

Masuala ya UM

“Ni wakati wa kupiga kengele ya dharura”, amesema Katibu Mkuu wa UN katika mahojiano maalum na Idhaa ya Umoja wa Mataifa siku chache kabla ya kuanza kwa Mjadala wa Juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Akihojiwa na Assumpta Massoi wa UN News, António Guterres amegusia ushirikiano wa kimataifa, harakati za utoaji wa chanjo dhidi ya COVID-19 duniani, mabadiliko ya tabianchi, usawa wa jinsia, viijana, amani na usalama barani Afrika na duniani kwa ujumla.