Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

UN News

Mahojiano la Mbunge Neema Lugangira wa Tanzania kuhusu nafasi ya mbunge kwa umma

Uwepo wa wabunge wenye nguvu ni msingi imara wa Demokrasia kwa mujibu wa lengo namba 16 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs ya Umoja wa Mataifa linalolenga amani, haki na taasisi thabiti. Hilo ni dhahiri kwa kuwa wawakilishi hao wa wananchi wanakuwa na uwezo wa kutunga sheria, kutenga fedha kwenda kufanya kazi ya utekelezaji wa sheria na sera walizozipitisha na kuwajibisha serikali iwapo haijatenda yale wananchi wanayakusudia kwa kuzingatia makundi yote kwenye jamii hususan walioko kwenye mazingira magumu. 

Kuelekea siku ya kimataifa ya Mabunge 30 Juni, Leah Mushi amefanya mahojiano na mbunge wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, kuhusu nafasi ya wabunge katika kuhakikisha usalama wa wananchi wao hususani wakati huu dunia ikipambana na janga la corona au COVID19. kwanza anaanza kwa kujitambulisha 

Sauti
8'51"
UNPA imetoa mabango ya kuonesha mshikamano wa kupinga ubaguzi
UNPA

Ni wakati wa kubadili mwelekeo kukomesha ubaguzi wa rangi wa kimfumo: Bachelet

Kamishia Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet leo ametoa wito wa haraka kwa nchi kupitisha "ajenda ya mabadiliko ili kung'oa ubaguzi wa kimfumo, kama alivyochapisha ripoti ikitoa mwangaza juu ya ukiukaji wa haki za kiuchumi, kijamii, kitamaduni, kiraia na kisiasa unaowakabili  watu wa asili ya Kiafrika kila siku katika mataifa tofauti.” 

Nyuso za furaha kutoka kwa wanakikundi cha Ushindi mkoani Kigoma baada ya mavuno bora kufuatia mafunzo ya mbinu bora za kilimo kutoka FAO ambazo walitumia kwenye shamba darasa.
FAO Tanzania

Ripoti ya FAO yaangazia vitisho dhidi ya mifumo ya chakula ya watu wa asili 

Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO, pamoja na kituo cha kimataifa cha utafiti wa kilimo kwa nchi za kitropoki, CIAT,  wametoa leo utafiti mpya unaotambulisha mamia ya aina mbalimbali za mimea na wanyama ambazo watu wa asili ulimwenguni wanategemea na kutunza ili kuzalisha chakula endelevu na kuongeza baiyonuai na pia wametoa onyo la kuongezeka kwa vitisho dhidi ya mifumo hii ya ya chakula. 

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina Mohammed akihutubia katika katika chuo kikuu Mjini Abuja nchini Nigeria
UNIC Lagos/Oluseyi Soremekun

Suluhisho pekee la migogoro na vita ni kuizuia:Amina J Mohammed

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J Mohammed amesisitiza umuhimu wa mtazamo wa kuzuia, katika kutatua changamoto za migogoro na vita kote duniani akisema “Suluhisho pekee na endelevu kwa changamoto za migogoro ni kuzuia. Kuzuia kutatusaidia kunyoosha pindo lililopo sasa la vita na machafuko na hivyo kutoa fursa kwa nyenzo zetu za kudhibiti maigogoro ambazo mara nyingi zinazidiwa uwezo.” 

IMO yataka mabaharia wachukuliwe kama wafanyakazi muhimu wa msitari wa mbele
IMO

Mabaharia ni wafanyakazi muhimu na wa msitari wa mbele wanaostahili kupewa haki:UN 

Leo ni siku ya mabaharia duniani na katibu mkuu wa shirika la kimataifa la masuala ya bahari IMO Kitack Lim amesema mabaharia siku zote wamekuwa kitovu cha biashara duniani na kazi yao inagusa maisha ya kila mtu iwe ni chakula kinawekwa mezani kwetu, dawa zinazodumisha afya ya kila mtu, kompyuta zinazotumika kwa kazi au kujiburudisha au magari yanayotusafirisha kila siku.