Tanzania tumejiunga na COVAX ili tupate chanjo ya COVID-19; idadi ya wagonjwa ni zaidi ya 100- Rais Samia
Wakati shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO kanda ya Afrika likionya kuwepo kwa wimbi la tatu la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 barani Afrika, Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema sasa taifa hilo lina wagonjwa zaidi ya 100 na tayari taratibu zinafanyika ili kuingiza chanjo ya COVID-19.