Skip to main content
Karibu Umoja wa Mataifa
Lugha
  • العربية
  • 中文
  • English
  • Français
  • Русский
  • Español
  • Português
  • Kiswahili
  • Nyingine
    • Hindi हिंदी
    • duniani
Umoja wa Mataifa
Habari za UN
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Search the United Nations

Tafuta Zaidi
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
  • Mwanzo
    • Afrika
    • Amerika
    • Asia Pasifiki
    • Mashariki ya Kati
    • Ulaya
  • Mada
    • Amani na Usalama
    • Ukuaji wa Kiuchumi
    • Msaada wa Kibinadamu
    • Tabianchi na mazingira
    • Haki za bindamu
    • Masuala ya UM
    • Wanawake
    • Sheria na Kuzuia Uhalifu
    • Afya
    • Utamaduni na Elimu
    • SDGs
    • Wahamiaji na Wakimbizi
  • Kwa kina
    • Habari kwa Picha
    • Mahojiano
    • Makala
    • Neno La Wiki
    • Makala Maalum
    • Videos
    • Siku za UN
  • Katibu Mkuu
    • Msemaji wa Katibu Mkuu
    • Taarifa zote
    • Hotuba muhimu
    • Mikutano na wanahabari
    • Safari za kikazi
  • Vyombo vya Habari
    • Video za Umoja wa Mataifa
    • Picha za Umoja wa Mataifa
    • Matukio ya Mikutanoni
    • Usajili kwa wanahabari
    • Webtv
 

Sajili

Kabrasha la Sauti

Kumekuwa na ongezeko la watu wazima wanaotumia dawa za kulevya.
Unsplash/Cristian Newman
Kumekuwa na ongezeko la watu wazima wanaotumia dawa za kulevya.

Tutumie takwimu za kisayansi kupambana na matumizi ya Dawa za Kulevya: Guterres

26 Juni 2021
Sheria na Kuzuia Uhalifu

Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Antonio Guterres ameziasa nchi wanachama kuhakikisha zinatumia takwimu zinazotolewa na wanasayansi katika kufanya maamuzi yao ili kuokoa maisha ya wananchi wengi zaidi akitolea mfano namna sayansi ilivyoweza kuleta afueni kwenye mapambano ya janga la Corona au COVID-19.

Kupitia ujumbe wake wa Siku ya kimataifa ya udhibiti wa dawa ya Kulevya na kuzuia usafirishaji haramu akiwa mjini New York Marekani Guterres amesema, ingawa maambukizi ya virusi vya ukimwi yamepungua lakini takwimu za watu wanaotumia dawa za kulevya hazijapungua.
“Ripoti mpya iliyotolewa wiki hii na Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusika na Madawa na Uhalifu – UNODC imeonesha vifo vitokanavyo na matumizi ya dawa za kulevya vimeongezeka katika muongo uliopita. Maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi kwa watu wazima duniani kote yamepungua kwa miaka ya hivi karibuni, lakini sio kwa watu wanaojichoma dawa za kulevya, ambao wanafikia asilimia 10 ya waathirika wapya kwa mwaka 2019. “
Guterres amesema ingawa nchi zinashirikiana kudhibiti usafirishaji haramu wa dawa za kulevya lakini nchi nyingi zenye kipato cha chini zina mifumo dhaifu ambayo inaruhusu biashara hiyo kuendelea. Pia amegusia suala la dawa zinazo dhibitiwa matumizi yake.
“kuna utofauti mkubwa sana kwenye nchi zenye kipato cha chini na cha kati katika suala la upatikanaji wa dawa muhimu zinazodhibitiwa. Kwa mfano, wataalamu wa matibabu Afrika Magharibi na Kati katika mwaka 2019 walikuwa na wanatoa dozi 4 za dawa za maumivu kila siku kwa wakazi Milioni Moja, Wakati Amerika ya Kaskazini idadi ya vipimo ilikuwa karibu 32,000”
Pia ameshauri vyombo vya ulinzi na usalama kuwasaka wahusika wakuu wa usafirishaji wa dawa za kulevya badala ya kuwakamata tuu watumiaji iwapo wanataka kumaliza tatizo hili katika nchi zao. 
Katibu Mkuu Guterres amezihimiza nchi wanachama kutumia takwimu kutafuta suluhu, “uwepo wa takwimu bora utasaidia kutambua mwenendo na kuwezesha ufuatiliaji wa wakati halisi wa njia za usafirishaji zinazohama haraka. Mifumo ya kutoa tahadhari mapema ya kisayansi itasaidia kutabiri vitisho vitakavyo ibuka vya dawa za kulevya” 

 

Mtumiaji wa mihadarati akitumia dawa  mbadala kwa ajili ya kuondowa hamu ya mihadarati
Picha/IRIN/Sean Kimmons
Mtumiaji wa mihadarati akitumia dawa mbadala kwa ajili ya kuondowa hamu ya mihadarati

 

   Ripoti ya UNODC imesemaje?

 

Mapema wiki hii Mkurugenzi mtendaji wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusikana Madawa na Uhalifu – UNODC Ghada Waly alitoa ripoti iliyoonesha idadi ya watu wanaotumia mihadarati duniani imeongezeka na kwamba mwaka 2020 pekee duniani kote watu milioni 275 walitumia mihadarati ikiwa ni ongezeko la asilimia 22. 
Waly amesema sasa wanaendesha kampeni ya #Onesha Takwimu za dawa za kulevya. Okoa Maisha kwakuwa takwimu za watumiaji wa dawa hizo haramu wanapoteza maisha na kuondoa nguvu kazi ya dunia inazidi kuongezeka. 

“Zaidi ya watu milioni 36 wamepata shida kutokana na utumiaji wa dawa za kulevya, dawa hizi zimesababisha vifo vya takriban watu nusu milioni kwa mwaka 2019. Kampeni hii inalenga kuelimisha Umma, watoa maamuzi na wahudumuwa afya umuhimu wa kufanya maamuzi kwa kutumia takwimu halisi zinazo onesha ukubwa wa tatizo” amesema Mkurugenzi huyo mtendaji wa UNODC

 Pia mkurugenzi huyu amesisitiza umuhimu wa nchi kufanya maamuzi ya kudhibiti kwa kutumia taarifa na takwimu za kisayansi ili waweze kukabiliana na matumizi ya dawa za kulevya ambayo kwa upande wa watumiaji wake kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi hayajapungua. 
“Tufanye habari zilizo hakikiwa kuwa ndio mshirika wetu wakati huu tunapo shughulikia changamoto za dawa za kulevya ulimwenguni na tufanye uwajibikaji wa pamoja wakati tukiwa na maono ya kuhakikisha kila mmoja wetu anakuwa na afya njema”
 

 

♦ Kupata takwimu za waathirika vitani Ukraine bofya  hapa.
♦ Iwapo ungependa kupokea taarifa kutoka UN News Kiswahili kila wakati zinapochapishwa jisajili  hapa.
♦ Pia unaweza kupakua apu ili kusikiliza matangazo yetu wakati wowote popote ulipo.
♦ Tembelea pia chaneli yetu ya Youtube na pia Soundcloud na Twitter
Dawa za kulevya|#Usafirishaji haramu|Matumizi ya Dawa|Siku za Umoja wa Mataifa

Taarifa Zihusianazo

Dawa za kulevya

Hatuwezi kuruhusu tatizo la mihadarati kuendelea kuathiri mamilioni ya watu:Guterres

Tayari kuna mfuko maaalum wa kusaidia manusura wa usafirishaji haramu, mfuko huu uko chini ya UNODC

COVID-19 yatumbukiza zaidi watu katika mtego wa kusafirishwa kiharamu- UNODC

Tokomeza usafirishaji wa binadamu. Kwa mujibu wa ripoti ya kimataifa ya UNODC asilimia 30 ya watu wanaosafirishwa kiharamu ni watoto.

Hatua zaidi zinahitajika kukabiliana na usafirishaji haramu kwenye mizozo-UNODC

Maktaba

  • Taarifa kwa watangazaji
  • Viunganishi vya Umoja wa Mataifa
  • Angalizo
  • UN Journal
  • Taarifa za Habari
  • Mikutano
  • Maktaba ya Picha na Video
  • Wasiliana nasi

Katibu Mkuu

  • Taarifa zote
  • Safari za kiofisi
  • Kona ya wanahabari
  • Kutoka Twitter ya Katibu Mkuu

Msemaji wa UN

  • Nyaraka zote
  • Muhtasari wa mkutano na wanahabari
  • Maandishi ya mkutano na wanahabari
  • Taarifa kwa wanahabari

Tupate

  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • RSS
  • Mawasiliano
  • Rambaza
  • Washirika wetu kwa sasa
Umoja wa Mataifa
Changia
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • Soundcloud
  • Podcast
  • UN Social Media
  • A-Z Site Index
  • Hakimiliki
  • Maswali ya mara kwa Mara
  • Fraud Alert
  • Privacy Notice
  • Kanuni za matumizi
  • Facebook
  • Twitter
  • YouTube
  • SoundCloud
  • Podcast
  • More Socials