UNHCR yakaribisha sheria mpya ya kuomba hifadhi Chad
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limeipongeza serikali ya Chad kwa kupitisha kwa mara ya kwanza sheria ya kuomba hifadhi ambayo itaimarisha ulinzi kwa karibu wakimbizi 480,000 wanaohifadhiwa nchini humo hivi sasa.