Skip to main content
Wahudumu wa kiafya katika hospitali ya tiba ya Chuo Kikuu cha Nanjin nchiin china wakishauriana na mgonjwa kuhusu upasuaji wa kupandikiza pafu.

Virusi vilivyotikisa dunia: 2020, mwaka tofauti na mingine

Chen Jingyu
Wahudumu wa kiafya katika hospitali ya tiba ya Chuo Kikuu cha Nanjin nchiin china wakishauriana na mgonjwa kuhusu upasuaji wa kupandikiza pafu.

Virusi vilivyotikisa dunia: 2020, mwaka tofauti na mingine

Afya

Ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona au COVID-19 uko kila pahali na katika mwaka 2020 ulisambaa na kuleta madhara makubwa yaliyosababisha janga la dunia ambalo mapana yake hayakutarajiwa. Katika mfululizo wa makala sita juu ya mwaka huu wa mtikisiko, UN News inamulika athari za ugonjwa huu kwa watu kwenye maeneo mbalimbali ya dunia na suluhisho ambazo Umoja wa Mataifa umependekeza kufuatia janga hili. Katika makala hii ya kwanza tunamulika mambo ya msingi katika miezi 12 ya mwaka huu wa 2020.

 

Hospitali kwenye ukanda wa Gaza huko Mashariki ya Kati wakati COVID-19 ilipokuwa imeshika kasi.
WHO
Hospitali kwenye ukanda wa Gaza huko Mashariki ya Kati wakati COVID-19 ilipokuwa imeshika kasi.

Mwaka 2020 unavyofunga pazia, na watu kila kona ya dunia wakitathmini jinsi ambavyo dunia imebadilika, wanakabiliwa na takwimu za kutisha. Idadi ya watu ambao wamekufa baada ya kuambukizwa COVID-19 inanyemelea milioni mbili. 

Abiria wakiwa wamevaa barakoa na makoti ya nailoni au poncho, wakikaguliwa hati zao za kusafiria kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Don Mueng huko Bangkok, Thailand.
UN News/Jing Zhang
Abiria wakiwa wamevaa barakoa na makoti ya nailoni au poncho, wakikaguliwa hati zao za kusafiria kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Don Mueng huko Bangkok, Thailand.

Mapema mwaka huu, safari za kimataifa zilikumbwa na vikwazo vikubwa, watu kama wasafiri hawa nchini Thailand walitambua umuhimu wa kuvaa vazi la kujikinga mwili mzima, PPE, vazi ambalo sasa limejipatia umaarufu duniani.

Shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP nchini China limepatia serikali ya China vifaa muhimu vya matibabu.
UNDP China
Shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP nchini China limepatia serikali ya China vifaa muhimu vya matibabu.

Punde, hofu ilitanda kuhusu uhaba wa mavazi hayo, PPE, na Umoja wa Mataifa ulisaidia nchi kadhaa katika ununuzi wa vifaa hivyo ikiwemo China ambako virusi hivyo vilianzia.

Ofisi ya daktari wa meno kwenye eneo la Brooklyn jijini New York, ikiwa imeweka bango la kukumbusha mabadiliko machungu ambayo yameletwa na virusi vya Corona.
UN News/Daniel Dickinson
Ofisi ya daktari wa meno kwenye eneo la Brooklyn jijini New York, ikiwa imeweka bango la kukumbusha mabadiliko machungu ambayo yameletwa na virusi vya Corona.

Kadri COVID-19 ilivyozidi kushika kasi, nchi na maji nayo duniani kote ilianza kuweka vikwazo vya matembezi, shule zikafungwa, shughuli za michezo na kitamaduni halikadhalika bila kusahau biashara ambazo zilionekana kuwa hazina umuhimu.

Jiji la Nairobi, Kenya
World Bank/Sambrian Mbaabu
Jiji la Nairobi, Kenya

Kwa kawaida, miji yenye kukurukakara nyingi kama vile mji mkuu wa Kenya, Nairobi, ulikuwa kimya kwa kuwa watu walilazimika kusalia majumbani.

Wajumbe katika ukumbi wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa wanazingatia umbali kati ya mtu na mtu wakati mikutano inayoendelea katika Umoja wa Mataifa
UN Photo/Eskinder Debebe)
Wajumbe katika ukumbi wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa wanazingatia umbali kati ya mtu na mtu wakati mikutano inayoendelea katika Umoja wa Mataifa

Umoja wa Mataifa ulisalia wazi ukiendelea na majukumu yake duniani kote, ijapokuwa matukio muhimu kama vile mkutano wa kila mwaka wa mjadala wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwenye makao makuu New  York, Marekani ulifanyika kwa njia tofauti. Ni wajumbe wachache tu ambao waliruhusiwa kuingia kwenye vyumba vya mkutano huku marais na viongozi wakuu wa nchi wakihutubia kwa njia ya mtandao.

Umbali ili kuepuka kuchangamana ukishuhudiwa nchini Yemen, na hii itahitajika kuendelea duniani kote, angalau hadi chanjo itakapokuwa imekamilika.
MFD/Elyas Alwazir
Umbali ili kuepuka kuchangamana ukishuhudiwa nchini Yemen, na hii itahitajika kuendelea duniani kote, angalau hadi chanjo itakapokuwa imekamilika.

Dunia kote watu walianza sasa kuzingatia kanuni mpya za kutochangamana, kuhakikisha umbali wa futi  6 kati ya mtu na mtu iwe shuleni, madukani au kwingineko kwenye huduma. …..

Wafanyakazi wa kijamii wanaowezeshwa na Umoja wa Mataifa, wakihamasisha umma kuhusu mbinu za kujikinga na COVID-19 na kusambaza vifaa vya kujisafi miongoni mwa kaya maskini nchini Bangladesh.
UNDP Bangladesh/Fahad Kaize
Wafanyakazi wa kijamii wanaowezeshwa na Umoja wa Mataifa, wakihamasisha umma kuhusu mbinu za kujikinga na COVID-19 na kusambaza vifaa vya kujisafi miongoni mwa kaya maskini nchini Bangladesh.

…na watu walikumbushwa kuhusu umuhimu wa kunawa mikono kama njia mojawapo ya kupunguza maambukizi ya magonjwa.

Samuel, 11 na mdogo wake wa kike Janet 10, wakisoma nyumbani kwao Mathare, Nairobi Kenya wakitumia meza pekee iliyoko ndani mwao na pia simu ya familia yao.
© Alissa /Everett
Samuel, 11 na mdogo wake wa kike Janet 10, wakisoma nyumbani kwao Mathare, Nairobi Kenya wakitumia meza pekee iliyoko ndani mwao na pia simu ya familia yao.

Wanafunzi ambao hawakuweza kwenda shule, walilazimika kuzoea ukweli mpya wa jinsi ya kuendelea na masomo yao wakiwa nyumbani.

Wanawake nchini Nigeria wakipokea mgao wa vocha za chakula kama sehemu ya programu ya kusaidia familia zinazohaha wakati huu wa COVID-19 na hatua za kudhiiti kusambaa kwa ugonjwa huo.
WFP/Damilola Onafuwa
Wanawake nchini Nigeria wakipokea mgao wa vocha za chakula kama sehemu ya programu ya kusaidia familia zinazohaha wakati huu wa COVID-19 na hatua za kudhiiti kusambaa kwa ugonjwa huo.

Wakati Afrika ilionekana kutopata madhara makubwa kutokana na virusi vya Corona ikilinganishwa na mabara mengine, kwa kuzingatia idadi ya maambukizi na vifo, Umoja wa Mataifa ulipaza sauti kuwa gonjwa hilo litatumbukiza watu wengi zaidi kwenye umaskini.

Mhudumu wa afya akitoa huduma Cox's Bazar nchini Bngladesh.
IOM/Nate Webb
Mhudumu wa afya akitoa huduma Cox's Bazar nchini Bngladesh.

Jambo muhimu zaidi ni kwamba Umoja wa Mataifa ulikuwa unasaidia wakimbizi na makundi mengine yanayohamahama na yaliyo hatarini zaidi kama vile maelfu ya wakimbizi warohingya kutoka Myanmar waliosaka hifadhi kwenye mpaka na Bangladesh.

Chanjo dhidi ya COVID-19 iliyotengenezwa na Chuo Kikuu cha Oxford nchini Uingereza imeonesha kuwa na ufanisi katika majaribio kwa kuweza kuzuia watu kupata dalili za Corona.
University of Oxford/John Cairns
Chanjo dhidi ya COVID-19 iliyotengenezwa na Chuo Kikuu cha Oxford nchini Uingereza imeonesha kuwa na ufanisi katika majaribio kwa kuweza kuzuia watu kupata dalili za Corona.

Hadi sasa kuna maendeleo yamepatikana, katika rekodi ya aina yake, wanasayanasi wametengeneza chanjo fanisi dhidi ya COVID-19 na ifikapo mwishoni mwa mwaka huu, watu walishaanza kupatiwa chanjo hiyo katika nchi zilizoendelea.

Mkazi wa New York nchini Marekani akifanya uchechemuzi wa jinsi ambavyo anadhani mlipuko wa janga la Corona unaweza kushughulikiwa.
UN Photo/Evan Schneider
Mkazi wa New York nchini Marekani akifanya uchechemuzi wa jinsi ambavyo anadhani mlipuko wa janga la Corona unaweza kushughulikiwa.

Dunia inapoingia mwaka 2021, janga la Corona bado linatikisa, na baada ya angalau nusu mwaka ya ukimya, bado maambukizi na vifo vinaripotiwa. Jinsi chanjo zaidi zinavyozidi kutengenezwa, jamii ya kimataifa inaombwa kushirikiana ili kuepusha kusambaa zaidi kwa virusi hivyo na kufuata miongozo ya kisayansi.
Kwa taswira zaidi ya mwaka 2020, endelea kufuatilia mfululizo wa makala hizi maalum kadi mwaka unavyoyoyoma.