Tufanye kila tuwezalo kupunguza mateso ya watu wa Palestina-Katibu Mkuu wa UN
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake wa siku ya mshikamano na Wapalestina ametoa wito kwa dunia kujitolea upya kusaidia Wapalestina katika harakati zao za kufikia haki zao na kujenga mustakabali wa amani, utu, haki na usalama.