Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mabadiliko ya tabianchi ni moja ya changamoto zinazoikabili dunia. Mathalani ukanda wa Sahel kusini mwa jangwa la Sahara.
© UNDP Mauritania/Freya Morales

Huwezi kuyavalia barakoa mabadiliko ya tabianchi, pia hayana chanjo-Andrew Harper 

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, kesho Jumatano likifanya mkutano wa ngazi ya juu kushughulikia athari za mabadiliko ya tabianchi kwa wakimbizi na wakimbizi wa ndani, pamoja na wengine walio katika mazingira hatarishi kote, mshauri maalumu wa UNHCR kuhusu mabadiliko ya tabianchi Andrew Harper amesema dunia inapaswa kuchukua hatua kali zaidi kwani mabadiliko ya tabia nchi huwezi kuyavalia barakoa. 

Sauti
1'49"
Mbu aina ya anopheles waambukizao malaria wakiwa katika maabara ya taasisi ya KEMRI/CDC nje ya mji wa Kisumu nchini Kenya
Sven Torfinn/WHO 2016

Ripoti mpya ya malaria yatoa wito wa kuchukuliwa hatua mpya za mapambano

Kwa mujibu wa ripoti mpya ya malaria ulimwenguni iliyotolewa hii leo na shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, maendeleo dhidi ya malaria yanaendelea kupungua, hasa katika nchi zenye mzigo mkubwa barani Afrika. Mapengo katika upatikanaji wa zana za kuokoa maisha yanadhoofisha juhudi za ulimwengu za kukabiliana na ugonjwa huo, na janga la COVID-19 linatarajiwa kurudisha nyuma zaidi mapambano.