Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Takribani saa sita mchana ya tarehe 9 Agosti 1945, bomu la nyuklia liliangushwa na Marekani kwenye mji wa Nagasaki na wingu zito lilienea mjini humo, picha hii ilipigwa  umbali wa kilometa 3 kutoka kitovu cha bomu hilo.
UN /Nagasaki International

Mkataba wa UN wa kutokomeza nyuklia kuanza kutumika Januari mwakani: Guterres asema ni hatua ya kipekee

Hatimaye mkataba wa kimataifa wa kupinga matumizi ya silaha za nyuklia, TPNW, utaanza kutumika tarehe 22 mwezi Januari mwaka ujao wa 2021 baada ya Honduras kuwa mwanachama wa 50 wa Umoja wa Mataifa kuridhia mkataba huo jana jumamosi, hatua ambayo imeelezewa kuwa zama mpya ya kutokomeza silaha za nyuklia duniani.

 

Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Kennedy Gastorn akihutubia Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo Jumanne Septemba 29, 2020
UN /Loey Felipe

Tunashukuru kwa usaidizi dhidi ya COVID-19, sasa maisha yamerejea hali ya kawaida- Tanzania

Tanzania imezungumza kwenye mjadala mkuu wa mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kuelezea msimamo wake katika masuala mbalimbali ikiwemo ushirikiano wa kimataifa, janga la ugonjwa wa Corona, COVID-19, amani na usalama maziwa makuu na mustakabali wa Umoja wa Mataifa wakati huu ambapo chombo hicho kinatimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake.

 

Sauti
2'59"
Volkan Bozkri, Rais wa mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la UN, UNGA75 akinyanyua rungu kuashirikia kuchukua urais wa kiti hicho, huku Katibu Mkuu Antonio Guterres na Rais aliyemazali muda wake Tijjani Muhammad-Bande wakitazama.
UN WebTV

Kwaheri UNGA74 karibu UNGA75

Hatimaye mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umefunga rasmi pazia lake hii leo na kuashiria kuanza kwa mkutano wa 75 wa Baraza hilo, ambalo ni moja vyombo vikuu vya Umoja wa Mataifa wenye wanachama 193.