Miaka 20 ya azimio namba 1325: Mafanikio na Changamoto
Mwaka huu azimio namba 1325 la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu wanawake na ulinzi na usalama duniani, limetimiza miaka 20 tangu kupitishwa kwake.
Mwaka huu azimio namba 1325 la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu wanawake na ulinzi na usalama duniani, limetimiza miaka 20 tangu kupitishwa kwake.
Hatimaye mkataba wa kimataifa wa kupinga matumizi ya silaha za nyuklia, TPNW, utaanza kutumika tarehe 22 mwezi Januari mwaka ujao wa 2021 baada ya Honduras kuwa mwanachama wa 50 wa Umoja wa Mataifa kuridhia mkataba huo jana jumamosi, hatua ambayo imeelezewa kuwa zama mpya ya kutokomeza silaha za nyuklia duniani.
Leo ni siku ya Umoja wa Mataifa ikiwa ni maadhimisho ya miaka 75 tangu kuanzishwa kwa chombo hicho mwaka 1945 huko San Francisco nchini Marekani wakati huu wanachama waanzilishi wakiwa ni 50.
Kamati ya tuzo ya amani ya Nobel yenye makao yake nchini Norway leo imelitangaza shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP kuwa ndio mshini wa tuzo ya amani ya Nobel kwa mwaka huuu wa 2020.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesema kitendo cha serikali ya mpito na waasi nchini Sudan kutia saini mkataba wa amani kinaashiria mwanzo wa zama mpya kwa wananchi wa taifa hilo.
Tanzania imezungumza kwenye mjadala mkuu wa mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kuelezea msimamo wake katika masuala mbalimbali ikiwemo ushirikiano wa kimataifa, janga la ugonjwa wa Corona, COVID-19, amani na usalama maziwa makuu na mustakabali wa Umoja wa Mataifa wakati huu ambapo chombo hicho kinatimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake.
Katika ukanda wa Sahel, ufugaji ndio chanzo kikuu cha kipato kwa zaidi ya wakazi milioni 20 wa eneo hilo ambao hata hivyo leo hii asilimia 40 ya watu hao wako kwenye lindi la umaskini na waliosalia wako hatarini kutumbukia kwenye umaskini.
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Félix Tshisekedi amehutubia mjadala mkuu wa mkutano wa 75 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa akieleza kuwa janga la Corona, COVID-19 ambalo pamoja na kusababisha vifo, limekuwa kizingiti kikubwa kwa harakati mbalimbali duniani.
Umoja wa Mataifa ukitimiza miaka 75 mwaka huu wa 2020 tangu kuanzishwa kwake, Tanzania, moja ya nchi 193 wanachama imesema chombo hicho hakina mbadala licha ya changamoto inazokikabili.
Hatimaye mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa umefunga rasmi pazia lake hii leo na kuashiria kuanza kwa mkutano wa 75 wa Baraza hilo, ambalo ni moja vyombo vikuu vya Umoja wa Mataifa wenye wanachama 193.