Vifo na uharibifu wa kimbunga Kenneth Comoro na Msumbiji vimenishtua:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ripoti za vifo na uharibifu mkubwa uliosababishwa na kimbunga Kenneth nchini Msumbiji na Comoro zimemshtua na kutoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuongeza msaada wa fedha kukabiliana na mahitaji ya dharura na ya muda mrefu ya waathirika.