Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wanawake katika jimbo la Copperbelt nchini Zam,bia wanaofanya kazi katika mfumo wa kilimo bora wanaongeza uzalishaji wa mbogamboga wanaouza katika masoko ya wenyeji( kutoka maktaba 2015)
ILO/Marcel Crozet

Usalama na afya kazini ni haki ya kila mtu:ILO

Katika kuadhimisha miaka 100 ya shirika la kazi ulimwenguni ILO ambalo dhamira yake ni kuhakikisha ajira bora na zenye hadhi kwa kila mtu, leo ikiwa ni siku ya usalama na afya kazini limetoa wito kwa serikali, waajiri na wafanyakazi kushiriki katika kujenga mazingira salama na yenye afya kazini.

Udongo wenye rutuba husaidia kilimo bora cha migomba kama vile mkoani Kagera nchini Tanzania
UNDP SGP Panama/Andrea Egan

Ulemavu sio kulemaa, ninachohitaji ni kuwezeshwa:Mkulima Gideon Masinde

Ingawa hali ya ulevu hasa wa viungo mara nyingi huleta changamoto kwa muhiska kuanzia  katika maisha ya kawaida na hata katika kujikwamua kiuchumi jambo ambao huwafanya wengi wasio na msaada kuishia kuwa ombaomba, au kukabiliwa na hali ngumu sana. Lakini kama walivyonena wahenga penye njia pana njia , kauli inayothibitishwa na Gideon Malungula Masinde mwenye umri wa miaka 42 ambaye ana ulemavu wa miguu yote na hawezi kusimama wa wala kutembea lakini hakuacha ulemavu wake umlemaze zaidi. 

Sauti
2'55"