Kinara wa UN azindua ajenda yake ya kudhibiti silaha duniani
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametangaza mwelekeo wake mpya kuhusu udhibiti wa silaha katika juhudi za kutokomeza silaha za nyuklia pamoja na silaha zingine zinazoweza kusababisha maangamizi dunia kutokana na makosa iwe ya kiufundi, kielektroniki au ya kibinadamu.