Mshauri mpya wa Kijeshi kwa DPKO amewasili Makao Makuu kuanza kazi
Liuteni Jenerali Chikadiba Obiakor wa Nigeria, Mshauri wa Masuala ya Kijeshi katika Idara ya UM Kuhusu Operesheni za Ulinzi wa Amani (DPKO) amewasili New York Alkhamisi kuanza kazi. Jenerali Obiakor amedhaminiwa madaraka ya kuishauri Idara ya DPKO juu ya masuala yote ya kijeshi yanayofungamana na shughuli za ulinzi amani za UM.