Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mjumbe wa KM kwa Usomali ajasirisha BU kudumisha amani haraka katika Pembe ya Afrika

Mjumbe wa KM kwa Usomali ajasirisha BU kudumisha amani haraka katika Pembe ya Afrika

Ahmedou Ould-Abdallah, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Usomali leo asubuhi alipohutubia mbele ya Baraza la Usalama juu ya hali katika Usomali aliwakumbusha wajumbe wa Baraza kuhusu wajibu walionao wa kuzingatia, kwa ujasiri mkubwa, uwezekano wa kubadili hadhi ya vikosi vya ulinzi wa amani vya UA vya AMISOM viliopo Usomali, ili vikosi hivyo vidhaminiwe madaraka mapya na viwe vikosi vya amani vya UM.