Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tume ya waliotoweka bila khiari duniani inakutana Argentina

Tume ya waliotoweka bila khiari duniani inakutana Argentina

Tume ya Utendaji ya UM juu ya Watu Waliolazimishwa Kutoweka na Kupotea Bila Khiari inakutana katika mji wa Buenos Aires, Argentina kuanzia Julai 24 mpaka 26 kufanya mapitio ya kesi za watu 300 waliotoweka duniani, kuambatana na matatizo ya kisiasa. Tume hiyo ina wajumbe wataalamu watano na inakutana, kwa mara ya kwanza katika taifa la Amerika ya Latina la Argentina, taifa ambalo katika miaka ya sabini na mwanzo wa miaka ya themanini liliathirika sana na tatizo la kupotea kwa wapinzani wingi wa kisiasa, bila ya aila zao kujua walipo.