Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ndege zilizobeba madawa ya kulevya zimekamatwa Guinea-Bissau

Ndege zilizobeba madawa ya kulevya zimekamatwa Guinea-Bissau

Kwenye taarifa iliotolewa na Shola Omoregie, Mjumbe wa KM kwa Guinea-Bissau iliripoti kushikwa kwa ndege mbili na watu wa usalama nchini Guinea-Bissau, ndege ambazo zinatiliwa shaka zimebeba shehena ya madawa ya kulevya. Kwa mujibu wa ripoti, baadhi ya watu wanaohusika na ndege hizo wamewekwa kizuizini kwa sasa wakisubiri matokeo ya uchunguzi juu ya fungamano walionayo na biashara ya madawa ya kulevya.