Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ECOSOC inazingatia uhusiano bora na mataifa yanayofufuka migogoro

ECOSOC inazingatia uhusiano bora na mataifa yanayofufuka migogoro

Baraza la Uchumi na Maendeleo la UM (ECOSOC), linalokutana Makao Makuu kwa sasa, linaeendelea na mijadala ya kuzingatia masuala maalumu ya kuimarisha uhusiano bora, na wa kuridhisha, na zile nchi zinazojitahidi kuibuka kutokana na athari na mabaki ya migogoro. ECOSOC pia inasialia taratizu za kupanua ushirikiano wake na ile Kamisheni ya UM juu ya Ujenziamani, kwa makusudio ya kuendeleza zaidi juhudi za muda mrefu za kufufua shughuli za kiuchumi na jamii kwenye maeneo husika.