Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mawaziri wa Maziwa Makuu wamekusanyika Kinshasa kuzingatia taasisi ya haki za wanawake

Mawaziri wa Maziwa Makuu wamekusanyika Kinshasa kuzingatia taasisi ya haki za wanawake

Mawaziri wanaohusika na haki za wanawake kutoka mataifa 11 ya Maziwa Makuu katika Afrika wameanza, Alkhamisi (24/07/08) mijadala ya siku mbili kwenye mji wa Kinshasa, katika Jamhuti ta Kideomkrasi ya Kongo (JKK) kuzingatia hatua za kuchukuliwa kipamoja kuanzisha taasisi mpya ya kikanda itakayoendeleza utafiti juu ya haki za kijinsiya na kushughulikia huduma za kuhifadhi nyaraka zinazoambatana na kadhia hiyo.