Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watumishi wa UM kuwakumbuka wenziwao waliouawa Algiers

Watumishi wa UM kuwakumbuka wenziwao waliouawa Algiers

Mapema wiki hii, mnamo tarehe 17 Disemba, watumishi wa UM walijumuika kote duniani kuwakumbuka wenziwao 17 waliouawa na shambulio la magaidi liliotukia Disemba 11 kwenye ofisi za UM mjini Algiers, Algeria. Wafanyakazi wa UM walikaa kimya kwa dakika moja kuheshimu kumbukumbu za wenziwao waliofariki Algiers.