UM yanuia kukomesha karaha ya utumiaji mabavu dhidi ya wanawake
KM wa UM Ban Ki-moon aliwasilisha risala maalumu, na muhimu, kwenye taadhima za kuiheshimu Siku ya Kimataifa ya Kukomesha Utumiaji Mabavu dhidi ya Wanawake. Jumuiya ya Kimataifa iliafikiana kuitambua tarehe 25 Novemba, kila mwaka, kuwa ni siku kuuzindua umma wa dunia juu ya jukumu kuu, na tukufu, la kupiga vita, kipamoja, vitendo karaha vya kutumia mabavu na nguvu dhidi ya watoto wa kike na wanawake.