Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mahakama ya ICC yasikiliza kesi yake ya kwanza mjini Hague

Mahakama pekee ya kudumu ya kimataifa juu ya makosa ya jinai ya vita, yaani Mahakama ya ICC ilisikiliza kesi yake ya mwanzo Alkhamisi, Novemba tisa(2006), iliofanyika mjini Hague, Uholanzi inayohusika na Thomas Lubanga Dyilo, aliyekuwa jemadari wa kundi la wanamgambo wa kundi la Forces Patriotiques pour la Liberation du Congo (FPLC) katika wilaya ya Ituri, Mashariki-kaskazini ya JKK katika miaka ya 2002-03.

Mashambulio na mauaji yaliyofanywa na wanamgambo karibuni katika Darfur yashtumiwa vikali na KM

KM Kofi Annan ametoa taarifa maalumu, kwa kupitia msemaji wake,iliyoshutumu vikali mashambulio ya hivi karibuni ya kundi moja la wanamgambo wa Sudan yaliyofanyika katika makazi ya eneo la Jebel Moon, Darfur ya Magharibi ambapo iliripotiwa makorja ya raia waliuawa, ikijumuisha pia watoto wadogo. Mashambulio haya yaliwalazimisha maelfu ya raia kuhajiri mastakimu kunusurisha maisha.