Maelfu ya wahamiaji wa Usomali wakimbilia Kenya kunusuru maisha
Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeripoti ya kuwa maelfu ya wahamiaji kutoka Usomali wanakimbilia Kenya hivi sasa kukwepa mapigano yaliofumka karibuni nchini mwao baina ya wafuasi wa Umoja wa Mahakama za Kiislamu (ICU) na vikosi vya Serekali ya Mpito.