Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashambulio na mauaji yaliyofanywa na wanamgambo karibuni katika Darfur yashtumiwa vikali na KM

Mashambulio na mauaji yaliyofanywa na wanamgambo karibuni katika Darfur yashtumiwa vikali na KM

KM Kofi Annan ametoa taarifa maalumu, kwa kupitia msemaji wake,iliyoshutumu vikali mashambulio ya hivi karibuni ya kundi moja la wanamgambo wa Sudan yaliyofanyika katika makazi ya eneo la Jebel Moon, Darfur ya Magharibi ambapo iliripotiwa makorja ya raia waliuawa, ikijumuisha pia watoto wadogo. Mashambulio haya yaliwalazimisha maelfu ya raia kuhajiri mastakimu kunusurisha maisha.