Kakuma yawa mwenyeji wa jukwaa la kwanza la kimataifa la TEDx kwenye kambi ya wakimbizi:UNHCR
Jukwaa la kwanza la kimataifa la TEDx kwa wakimbizi limefanyika Jumamosi kwenye kambi kubwa ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya
Jukwaa la kwanza la kimataifa la TEDx kwa wakimbizi limefanyika Jumamosi kwenye kambi kubwa ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya
Ajira bora na zenye hadhi zimetajwa kuwa ni chachu ya kuchagiza amani na mnepo katika jamii . Hayo yamesemwa na shirika la kazi duniani ILO kwenye mkutano wa 107 wa shirika hilo ambao leo umekuwa na kikao maalumu kilichobeba kauli mbiu “umuhimu wa ajira na ajira zenye hadhi kwa ajili ya amani na mnepo”na kujikita zaidi katika kukabiliana na hali halisi mashinani na pia katika ushirika ambao utazaa matunda.
Baada ya mashauriano ya muda mrefu, hatimaye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeridhia mapendekezo ya marekebisho ya mfumo wa maendeleo wa chombo hicho chenye wanachama 193. Marekebisho hayo yanalenga kusogeza zaidi UN kwa wananchi wa kawaida ili hatimaye maendeleo yawe dhahiri ya watu na si vitu.
Wakati dunia hivi sasa ikikabiliwa na changamoto chungu nzima zinazoongeza mzigo katika huduma za afya, iwe vita, majanga ya asili, mabadiliko ya tabia nchi na hata milipuko ya magonjwa hakuna kilicho muhimu kama kuwa na afya njema.
Barazani hii leo wajumbe wa wamejulishwa kuwa kwa kilichotokea huko ukanda wa Gaza, ni lazima kuchukua hatua za dhati ili kuepusha umwagaji zaidi wa damu.
Shirika la afya ulimwenguni WHO linapeleka timu ya wataalam 50 wa afya ya jamii nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ili kusaidia serikali kupambana na mlipuko wa Ebola. Patruck Newman na taarifa kamili
Guterres ataka shaka na shuku kwenye JCPOA iondolewe kwa kuzingatia mfumo uliowekwa na si kwa pande husika kujitoa kwenye makubaliano hayo yanayolenga kuwezesha Iran kuachana na nyuklia.
Kila sauti hiyo isikikapo wakati mama anajifungua huwa ni muziki masikioni mwake, lakini mamilioni ya watoto na kina mama duniani hupoteza maisha kila mwaka sababu ya kukosa dumuma bora wakati wa ujauzito, kipindi cha kujifungua na hata baada ya kujifungua, kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO.
Umoja wa Mataifa umetaka serikali kuzingatia uhuru wa vyombo vya habari kwa kuwa ndio msingi wa utawala bora na serikali zinazowajibika kwa umma.
Hatua ya kutoa mafunzo ya teknolojia ya habari na mawasiliano au TEKNOHAMA kwa wakimbizi kupitia shule ya ReDi nchini Ujerumani, imefufua matumaini ya mustakhbali wao waliokuwa wameukatia tamaa.