Kigeugeu kwenye mkataba wa kimataifa wa uhamiaji ni taswira mbaya kwa nchi husika:Abour
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya uhamiaji wa kimataifa Louise Abour amesema dhamira iliyowekwa bayana na nchi kadhaa ikiwemo Hungary, Poland , Jamhuri ya Czech na Australia ya kujiengua kwenye mkataba wa kimataifa wa wahamiaji inaonyesha picha mbaya kwao na ina athari kubwa katika ari ya ushirikiano wa kimataifa .