Azimio la kisiasa lapitishwa kuchochea afya kwa wote ifikapo 2030
Viongozi wa dunia leo wamepitisha azimio la kisiasa lenye lengo la kuhakikisha afya kwa wote ifikapo mwaka 2030.
Viongozi wa dunia leo wamepitisha azimio la kisiasa lenye lengo la kuhakikisha afya kwa wote ifikapo mwaka 2030.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antinio Guterres amesema mara nyingi dunia inaiangalia amani katika mtazamo wa migogoro baina ya binadamu. Lakini amani sio tu kutokuwa na vita, ni kutengeneza mazingira ya kuwa na utangamano na utulivu kwa njia ambayo watu wataishi pamoja na kuruhusu vita kutotokea.
Hatimaye kikao cha kwanza cha mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kimeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani chini ya uongozi wa Rais wake Balozi Tijjani Muhammad-Bande kutoka Nigeria.
Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ukianza rasmi leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, Rais mteule wa mkutano huo Balozi Tijjani Muhammad-Bande ametaja vipaumbele vyake vitatu kuwa ni umaskini, elimu bora na ujumuishaji wa kila mtu.
Kuelekea siku ya kimataifa ya kumbukizi ya manusura wa ugaidi, ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabiliana na ugaidi UNOCT imechukua hatua ya kupaza sauti za manusura hao kutoka maeneo mbalimbali duniani akiwemo mwanamke mmoja raia wa Cameroon ambaye anasema alilazimika kuwavisha mavazi ya kike watoto wake wa kiume ili wasichukuliwe na magaidi wa Boko Haram.
Katika kuadhimisha siku hii ya kimataifa ya huduma za kibinadamu , moja ya nchi ambayo inahitaji kwa hali na mali huduma hizo ni Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC, ambayo imeghubikwa na mjangamakubwa matano , kipindupindu, njaa, kutokuwa na uhakika wa chakula, vita nae bola.
Leo ni siku ya huduma za kibinadamu duniani ambapo Umoja wa Mataifa unapigia chepuo mwaka huu wanawake waliojikita katika kutoa huduma za kibinadamu kote ulimwenguni.
Leo katika mada kwa kina tunamulika kisa cha mwanamke mmoja nchini Kenya ambaye anasimulia madhila ya ukatili wa kiinsia.
Uganda ni moja ya nchi zilizo na idadi kubwa ya watu na idadi hiyo inaongezeka kila uchao. Kwa sasa nchi hiyo ina takriban watu milioni 40 na zaidi ya asilimia 75 wanaishi vijijini na asilimia 80 ya watu hao wako katika mashamba ya kurithi ambayo mengi hazijaandikishwa, kupimwa wala kuingizwa katika ramani.
Kasi ya maendeleo ya kupunguza maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi, VVU, kasi ya kuongeza wigo wa upatikanaji wa dawa na kupunguza vifo vitokanavyo na Ukimwi inapungua, imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na Ukimwi, UNAIDS.