Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nilianzisha shirika la kuwasaidia wanawake wajane baada ya mimi mwenyewe kuchungulia kaburi- Dianah Kamande 

Washiriki wa tukio la kuchagiza usawa wa kijinsia katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani mjini New York.
Photo: UN/Radmilla Suleymanova
Washiriki wa tukio la kuchagiza usawa wa kijinsia katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani mjini New York.

Nilianzisha shirika la kuwasaidia wanawake wajane baada ya mimi mwenyewe kuchungulia kaburi- Dianah Kamande 

Haki za binadamu

Leo katika mada kwa kina tunamulika kisa cha mwanamke mmoja nchini Kenya ambaye anasimulia madhila ya ukatili wa kiinsia.

Dianah Kamande ni mama wa watoto wawili nchini Kenya ambaye katika mazingira ya kushangaza, siku moja mume wake alirejea nyumbani akiwa na nia moja tu, kumuua mkewe, wanaye wawili na kisha yeye mwenyewe ajiue. Ingawa watoto walitoroshwa haraka, mama yao hakuwa na bahati hiyo kwani alikatwakatwa kwa mapanga kichwani na sehemu nyingi za mwili hivi sasa zimepandikizwa vyuma na mishipa ya bandia. 

Baada ya tukio hilo Dianah amebakia kuwa mjane kwani mume wake alijiua baada ya kufikiri kuwa ameshamuua mkewe. 

Sasa Dianah ameanzisha kundi la kuwaleta pamoja wajane ili wasaidiane katika masuala kadha wa kadha. Flora Nducha alifanya mahojiano na Bi Kamande alipokuwa mjini New York Marekani mapema mwaka huu kuhudhuria kikao cha kimataifa cha hali ya wanawake duniani.