Mengi yanayojadiliwa Baraza la Usalama yanahusu Afrika hivyo sauti ya Afrika ni muhimu- Kenya
Kenya ina uzoefu katika masuala ya Usalama na hiyo ni moja ya sababu ambayo imesukuma nchi hiyo ya Afrika Mashariki kuwania nafasi ya mwanachama asiye wa kudumu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.