Kila sekunde 40, kuna mtu anajiua-WHO
Kila sekunde 40, kuna mtu anajiua-WHO
Mtu mmoja hufariki dunia katika kila sekunde 40 kwa kujiua, limesema shirika la afya duniani hii leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya afya ya akili.
Siku hii ambayo huadhimishwa Oktoba 10 kila mwaka hutumika kukuza uelewa kuhusu afya ya akili na ujumbe wa mwaka huu ni kuzuia kujiua.
Takwimu za WHO zinaonesha kuwa kila sekunde 40, mtu mmoja mahali fulani duniani anafanya maamuzi ya kujiua uhai na watu takribani 800,000 wanajiua kila mwaka na hivyo kufanya matukio ya kujiua kuwa sababu ya pili katika sababu za vifo vya vijana wadogo wa umri wa miaka 15 na 29.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake kwa siku hii ya afya ya akili anasema, “afya ya akili imepuuzwa kwa muda mrefu lakini lakini inatuhusu sisi wote na hatua zaidi inahitajika haraka.”
Kujiua ni tatizo la afya ya umma. Leo #WorldMentalHealthDay chukua hatua kwa #40seconds kuchangia katika kupambana na tatizo hilo na kuonesha kwamba unajali.Soma zaidi: https://t.co/DyajXH5Hc6via @WHO pic.twitter.com/MHp5k36nD3
UmojaWaMataifa
Katibu Mkuu Guterres anataka ongezeko la uwekezaji katika huduma na anaongeza, “hatutakiwi kuruhusu unyanyapaa kuwazuia watu kuomba msaada wanaouhitaji.”
Kwa mujibu wa WHO kila kisa kimoja cha kujiua, kuna visa 20 vya majaribio ya kutaka kujiua na mara nyingi hurudiwa hadi kufanikiwa. Asilimia 80 ya visa vya kujiua hutokea katika nchi za chi za kipato cha chini na kati kutokana na ukosefu wa rasilimali za kutoa msaada na kumsaidia mtu ambaye ameathirika na msongo.
Katika siku hii, WHO inasisitiza kuwa kujiua kunaweza kuzuilika kwa kuunganisha jitihada na kuhusisha kila mtu katika jukumu hili.