Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

 Bandari ya uvuvi ya Joal nchini Senegal.
© FAO/Sylvain Cherkaoui

Shughuli za uvuvi na ufugaji wa Samaki zinatoa mchango mkubwa kwenye uhakika wa upatikanaji wa chakula :FAO

Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari ukiwa katika siku ya tatu hii leo huko Lisbon nchini Ureno Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limesema ongezeko kubwa la ufugaji wa samaki sambamba na uvuvi wa kimataifa umesababisha mazao ya vyakula vya majini kuwa kwenye rekodi ya juu katika kuchangia kwa kiasi uhakika wa chakula na lishe katika karne hii ya Ishirini na moja.

Sauti
2'26"
Amiri Juma Amiri mkulima huyu wa mwani akiwa na mwani aliovuna kutoka shambani kwake baharini kufuatia mradi unaofadhiliwa na taasisi ya utafiti wa majini na viumbe vya  bahari ya Kenya.
UN/ Kenya

Kilimo cha mwani baharini kimenitoa kwenye nyumba ya tope – Amiri wa Kibuyuni, Kwale - Kenya

Moja ya malengo ya Mkutano wa bahari unaoendelea Lisbon, Ureno, ni kujadili namna ambavyo dunia inaweza kuendelea kunufaika kiuchumi kutokana na uwepo wa bahari. Ajenda hiyo inakuwa muhimu kwa kuwa tayari ni dhahiri baharí imekuwa mkombozi wa kiuchumi kwa watu wengi duniani. Mfano wa wazi ni Amiri Juma Amiri, mkazi wa kijiji cha Kibuyuni katika Kaunti ya Kwale huko Pwani ya Kenya, mkulima wa zao la mwani ambalo hulimwa baharini.

Sauti
2'58"
UN Video

Vijana tunachagiza mabadiliko ya kisera ili kulinda bahari - Nancy Iraba

Mkutano wa pili wa kimataifa kuhusu bahari unaendelea huko Lisbon, Ureno. Mkutano huu umeanza tarehe 27 mwezi huu wa Juni na utamalizika tarehe 1 Julai 2022. Kabla ya kuanza kwa kikao cha ngazi ya juu, mkutano ulitanguliwa na jukwaa la vijana likileta pamoja wanaharakati na wachechemuzi vijana kuhusu masuala ya baharí wakionesha ubunifu wao wa jinsi ya kutatua dharura ya baharí, kama alivyooiita Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres .Miongoni mwa washiriki ni kijana Nancy Iraba mwanasayansi wa masuala ya bahari kutoka Chuo Kikuu cha Dare es salaam nchini Tanzania. Hapa akihoijwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa anaelezea jukwaa linajikita na nini.

Sauti
1'32"
Ufunguzi wa mkutano kuhusu bahari huko Lisbon, Ureno 27 Juni 2022
UN /Eskinder Debebe

Bahari inatupeleka popote, tuitunze- Guterres

Mkutano wa pili wa Umoja wa Mataifa kuhusu bahari umeanza leo huko Lisbon Ureno ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ni lazima kubadili mwelekeo na mwenendo wa shughuli za binadamu kwa bahari la sivyo uchafuzi wa bahari utavuruga harakati zote za kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs

Sauti
2'3"
Hema katika jangwa nchini Mauritania
Unsplash / Daniel Born

Sasa hatuna wasiwasi tena mvua isiponyesha:Wakulima Mauritania

Mabadiliko ya tabianchi yanaleta madhara kila kona ya dunia ikiwemo kupungua kwa viwango vya mvua na hivyo kuleta usumbufu mkubwa wa wakulima, mathalan nchini Mauritani kiwango cha mvua kilichokuwa kikinyesha miaka 30 iliyopita sasa wanapata robo tu ya kiwango hicho hali iliyowatesa wakulima na wafugaji lakini mradi wa Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya kilimo IFAD umewanusuru kwa kuwahakikishia maji mwaka mzima.

Sauti
2'23"
Mtoto majeruhi wa tetemeko la ardhi nchini Afghanistan akipata matibabu katika hospitali ya wilaya ya Urgun.
© UNICEF Afghanistan

Mamia ya watu wapoteza maisha kwenye tetemeko la ardhi Afghanistan UN yajipanga kusaidia

Wadau wa kimataifa wa misaada ya kibinadmu yakiwemo mashirika ya Umoja wa Mataifa wanajiandaa kusaidia maelfu ya familia zilizoathirika zaidi na tetemeko kubwa la ardhi lililokubwa majimbo ya Paktika na Khost nchini Afghanistan mapema leo, mamia ya watu wameripotiwa kufariki dunia, wengi kujerihiwa wengine vibaya sana huku miundombinu ikiharibiwa vibaya.

Sauti
2'16"
Kambini Kakuma
UN/Esperanza Tabisha

Wakimbizi tukikirimiwa tunarejesha fadhila kwa jamii:Bahati, Micheline na Agnes

Kutana na wakimbizi Bahati Hategekimana kutoka Rwanda, Micheline Muhima kutoka Uganda na Agnes Mude kutoka Sudan Kusini ambao wote walikuwa wakiishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya, lakini sasa kupitia mradi wa majaribio wa kuthamini mchango wa wakimbizi EMPP, unaoendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, mjini Pictou na serikali ya Canada watatu hao si wakimbizi tena bali ni wafanyakazi wa huduma ya jamii kwenye kituo cha Glen Haven Manor kilichopo jimboni Nova Scotia nchini Canada. 

Sauti
2'34"