Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Watu huyakimbia makazi yao mara kwa mara kaskazini-mashariki mwa Cameroon kutokana na migogoro.
UN Photo/Eskinder Debebe)

Mbinu za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi zaleta mapigano nchini Cameroon

Wakati Mkutano wa 26 wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya Tabianchi COP26 ukiwa umemalizika mwishoni mwa wiki huko Scotland huku Afrika ikisema haijafanikiwa ilivyotarajia, huko nchini Cameroon mabadiliko ya tabianchi yameleta uhasama baina ya wafugaji, wakulima na wavuvi, sababu kubwa ya ugomvi huo ni mbinu walizobuni za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
2'44"
Mtoto akipokea matibabu ya oksijeni katika hospitali katika Jimbo la Bengal Magharibi nchini India.
© UNICEF/Partha Mitra

Uchafuzi wa hewa wachochea nimonia: Oksijeni yahitajika

Kuelekea siku ya kimataifa ya kutokomeza ugonjwa wa Nimonia duniani, shirika la Umoja wa Mataifa la kufanikisha upatikanaji wa tiba nafuu UNITAID limetoa wito kwa washirika wote kuongeza kwa kasi ufadhili katika uzalishaji wa oksijeni na kujiunga na ubia wa kampeni ya  KILA PUMZI INAHESABIKA ili kuhamasisha kupunguza vifo vitokanavyo na uchafuzi wa hewa.

Sauti
2'11"